Waziri wa Kilimo Prof. Adolf Mkenda akiongea na Waandishi wa Habari mjini Moshi ambapo amesema makundi ya nzige yameendelea kudhibitiwa na kuwa hakuna madhara yaliyojitokeza kwenye mashamba ya wakulima hadi sasa (Picha na Wizara ya Kilimo)

…………………………………………………………………………………………………….

Waziri wa Kilimo Profesa Adolf Mkenda (Mb) ametoa tathmini ya kazi ya kuwadhibiti nzige wa jangwani waliovamia nchini mwanzoni mwa mwezi Januari mwaka huu na kuwa hadi sasa wamedhibitiwa na wataalam wa Wizara ya Kilimo kwa kushirikiana  na halmashauri za wilaya za Longido, Siha na Simanjiro.

Prof. Mkenda ameeleza hayo leo alipozungumza na waandishi wa habari Moshi mkoani Kilimanjaro kuwa mapambano dhidi ya nzige yanaendelea vizuri na kuwa hadi sasa hakuna madhara yoyote kwenye maeneo ya kilimo na mifugo ya wananchi na kuwa jitihada za kuangamiza makundi  yaliyobakia zinaendelea kwa kutumia helkopita na mabomba ya kupiliza kwa mikono.

“Tupo makini kuwakabili nzige hadi sasa hatujapata madhara yoyote kwa mashamba ya wakulima hivyo watanzania wasiwe na taharuki “alisisitiza Prof. Mkenda.

Kuhusu mikakati ya kupambana na nzige Waziri Mkenda amesema hadi leo tarehe 01 Machi tayari kuna helkopta kutoka Shirika la Nzige Wekundu (RLCO) na kuwa serikali itaongeza ndege ya pili kutoka shirika la Nzige wa Jangwani (DLCO) kupulizia makundi madogo ya nzige walionekana maeneo ya wilaya za Longido kufuatia uwepo wa taarifa kuwa nzige wachanga kutoka Kaunti ya Machakos nchini Kenya wanaweza ingia Longido.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...