Mchungaji wa kanisa la Waadventista Wasabato Magomeni, Baraka Butoke, akiongea na waandishi wa Habari akielezea dhumuni la ibada hiyo ya pamoja iliyofanyika katika kanisa la Waadventista Wasabato Magomeni. Leo Jumamosi 10/04/2021, Dar Es Salaam.
 
Mchungaji wa kanisa la Waadventista Wasabato Magomeni, Baraka Butoke akiongoza ibada kwa maombi, katika kanisa la Waadventista Wasabato Magomeni. Leo Jumamosi 10/04/2021, Dar Es Salaam.
 
Waimba kwaya wakiimba nyimbo za kumsifu na kumtukuza Mungu, katika kanisa la Waadventista Wasabato Magomeni. Leo Jumamosi 10/04/2021, Dar Es Salaam.
 
Waumini wakiwa wanasikiliza neno kutoka kwa Mcungaji Baraka Butoke, katika kanisa la Waadventista Wasabato Magomeni. Leo Jumamosi 10/04/2021, Dar Es Salaam
 
Wageni waalikwa kutoka Maeneo mbali mbali wakiwa wamekaa kujumuika katika ibada ya pamoja, katika kanisa la Waadventista Wasabato Magomeni. Leo Jumamosi 10/04/2021, Dar Es Salaam.
Wageni waalikwa kutoka Maeneo mbali mbali wakiwa wamekaa kujumuika katika ibada ya pamoja, katika kanisa la Waadventista Wasabato Magomeni. Leo Jumamosi 10/04/2021, Dar Es Salaam. 
 
********************
Na Mwandishi wetu.
Akizungumza na waandishi wa habari  Mchungaji wa kanisa la Waadventista Wasabato Magomeni, Baraka Butoke amesema, Leo ni sabato malaamu ambayo kanisa limeamua kujumuika na jamii inayotuzunguka katika kumuabudu Mungu na kula chakula kwa pamoja

Mchungaji Baraka Butoke amesema, Ni sabato ambayo tumealika marafiki zetu majirani zetu na watu ambao wanaoshi katika mazingira magumu hasa ambao sio waimani yetu, ili waje waone tunavyo abudu pia washiliki kula pamoja nasi na Kumsifu Mungu.

Aidha amesema, dhumuni hasa ni kuabudu pamoja na kula chakula pamoja, pia tumefanya mialiko maalumu kwa viongozi wa dini hasa kwenye makanisa na misikiti iliyopo katika eneo hili linalo tuzunguka, na wote kwa pamoja wamejumuika nasi katika iba hii ya leo.
 
"Pia tumealika watoto wanao wanao lelewa katika vituo vya kuleleaa watoto yatima na ambao wapo katika mazingira magumu ili waje washiriki na watoto wetu ili nao wahisi upendo kutoka kanisa hili." Aamesema. 
 
"Hii sio mara ya kwanza sisi kushirikiana na watu mbali mbali katika ibada ya pamoja mfano, kama sabato tatu zilizopita kulikua na kundi maalumu ambalo tulienda kuwatembelea huko walipo na kuwapelekea maitaji mbali mbali, na hii ni programu endelevu tutaendelea kushirikiana nao na kisaidiana nao tunawajenga kimwili lakini pia tunawajenga kiroho." Amesema.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...