NA DENIS MLOWE, IRINGA
MBUNGE wa Jimbo la Kalenga mkoani Iringa , Jackson Kiswaga amechangia,
shillingi
millioni 46 zilizotolewa na serikali kwa ajili ya mfuko wa jimbo lengo
la ujenzi wa miundo mbinu ya shule na ujenzi wa madarasa na mabweni
katika kata zote za Jimbo hilo.
Akizungumza
kwenye ofisi ya mkuu wa shule ya sekondari Lipuli , Mkurugenzi wa
halmashauri ya wilaya ya Iringa Vijijini Bashir Muhoja alisema kuwa
mbunge huyo ametoa fedha hizo za mfuko wa jimbo ambazo zimepelekea
kuunda bodi ambayo hadi sasa imekuwa ikiendelea na uboreshaji wa
miundombinu mashuleni.
Alisema kuwa mfuko wa jimbo na ni kitu ambacho kimeanzishwa na bunge na fedha hizi zinavyokuja zinakuwa na kamati yake
ndani
ya halmashauri na imepokea fedha za majimbo yote mawili Jimbo la Ismani
na Kalenga na baada ya kupitia vipaumbele na mahitaji ya husika.
Muhoja
alisema kuwa Mbunge Kiswaga alitazama mahitaji yanayotakiwa
kurekebishwa mapema kwanza ujenzi wa bweni la shule ya sekondari
Tanangozi na shule nyingine ndipo walipoelekeza fedha hizo zitumike.
Kwa
upande wake mbunge wa jimbo la Kalenga, Jackson Kiswaga alisema kuwa
nia ya serikali ni kuhakikisha inatatua changamoto zilizopo kwenye jamii
na kutokana na fedha walizozipata ikapelekea kuunda kamati ambayo
ilikuwa msaada kwa ajili ya uboreshaji wa miundombinu na madarasa
mashuleni.
Alisema
kuwa wanaishukuru serikali ya mama Samia Suluhu Hassan
rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambapo anaendelea
na kufanya utekelezaji wa ilani ya chama cha mapinduzi
kwa kuendelea kufikia lengo lililokusudiwa
“Katika
fedha ambazo huwa tunapatiwa mbunge huwa anaunda kamati na
tukaangalia vipaumbele kulingana na mahitaji tuliyonayo kwa
hiyo vipaumbele vyetu tulivyonavyo hasa kupunguza changamoto
tuliyonayo kwa upande wa madawati lakini pia kuna ujenzi mwingine
ambao unaendelea katika shule zetu pamoja na zahanati
.Kiswaga
alisema kuwa wananchi wawe na imani naye kwani bado yupo katika
utekelezaji wa miradi mbalimbali ambayo itasaidia kuleta maendeleo
katika jimbo hilo.
Naye
diwani wa kata ya Kalenga, Shakira Kiwanga alisema kuwa anashukuru kwa
utekelezaji unaoendelea pamojana kuahidi ujenzi kuanza mara moja kwani
vitendea kazi tayari vimeshatengwa
Alisema
kuwa viongozi watoe ushirikiano kwa kuwahamasisha wananchi kushiriki
katika maendeleo pamoja na kutambua kazi inayofanywa na mh.mbunge
kwani kwa kipindi cha nyuma katika shule ya sekondari
Isakalilo wanafunzi walikuwa wanaingia kwa awamu ambapo
changamoto hiyo imetatuliwa kutokana na fedha kiasi Cha sh
milioni .12 kusaidia kuboresha eneo hilo hasa kwenye madarasa.
Mbunge
Jackson Kiswaga amafanya utekelezaji huo kwa kutoa madawati 325 ambapo
kwa shule ya lipuli ametoa madawati 20 pamoja na saruji itakayosaidia
katika uboreshaji wa madarasa.
Mbunge wa Jimbo la Kalenga Jackson Kiswaga akimkabidhi mkuu wa Shule ya sekondari Lipuli,Peter Mbata saruji na vifaa mbalimbali kwa ajili ya ujenzi wa miundo mbinu ya shule hiyo.Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Iringa,Bashir Muhoja kulia akizungumza na mbunge wa Jimbo la Kalenga Jackson Kiswaga
Mbunge wa Jimbo la Kalenga Jackson Kiswaga akimkabidhi mkuu wa Shule ya sekondari Lipuli,Peter Mbata saruji na vifaa mbalimbali kwa ajili ya ujenzi wa miundo mbinu ya shule hiyo.Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Iringa,Bashir Muhoja kulia akizungumza na mbunge wa Jimbo la Kalenga Jackson Kiswaga
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...