Na Amiri Kilagalila, Njombe
Mwanafunzi
wa darasa la tatu shule ya msingi Ikelu iliyopo Makambako mkoani
Njombe, Claud Florence (9) amefariki dunia baada ya kujinyonga akiwa
anacheza na wenzake.
Kamanda
wa Polisi mkoa wa Njombe, Hamisi Issah amesema mwanafunzi huyo
alikwenda shambani na wazazi wake na wadogo zake watatu akiwa huko
alianza kucheza na wadogo zake na baadae kuchukua kikoi na kuanza
kujaribisha namna mtu anavyojinyonga.
Amesema
baada kufanya kitendo hicho katika mti pori uliopo hapo shambani
matokeo yake alijikuta amening'inia kwenye mti huo huku wazazi wakiwa
hawana taarifa yoyote wakiwa wanaendelea na kulima.
Amesema
wazazi walipofika walifungua hicho kikoi na kumkuta mtoto wao akiwa
taabani na kuchukua uamuzi wa kumpeleka hospitali na baadae kufariki
dunia.
Amewataka wazazi
kuwa makini na malezi ya watoto wao kwani malezi ya watoto ni pamoja na
kuangalia aina ya michezo wanayocheza katika mazingira yanayofaa.
"Watoto hawa wamecheza michezo ya kupitiliza mpaka wamejaribisha kujinyonga na mwenzao mmoja kajiua kabisa" amesema Issah.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...