Na Abdullatif Yunus Michuzi TV.

Ili kuendelea kuvutia Wawekezaji Mkoani Kagera na kuufanya Mkoa huo kuwa mahala sahihi na Salama kwa wawekezaji, Kituo Cha Uwekezaji Tanzania (TIC) Kimetembelea Kiwanda cha Kuchakata minofu ya Samaki aina ya Sangara cha Supreme Perch kilichopo Bukoba Manispaa eneo la Nyamkazi, ili kubaini shughuli za uendeshaji wa Kiwanda hicho.

Bi. Pendo Gondwe Mwakilishi wa TIC Kanda ya Ziwa akiambatana na wataalam wengine wamefika Kiwandani hapo mapema Februari 16 Mwaka huu na kufanya mazungumzo na Uongozi wa Kiwanda Hicho, kinachosimamiwa na Mwekezaji kutoka India, kabla ya kupata nafasi ya Kutembelea  na kukagua kiwanda hicho.

Meneja wa Kiwanda  Bwana Manoj Manohoran katika Mazungumzo hayo hakusita kuwasilisha changamoto zinazowakabili Kama Wawekezaji ikiwa ni pamoja na mifumo ya Kodi na Ushuru amabayo wamedai kutokuwa rafiki, Usumbufu wa Barabarani wakati wa kusafirisha samaki kilio kikubwa ikiwa ni kufunguliwa Mara kwa Mara mzigo wao na kupelekea kupoteza ubora, Ukosefu wa malighafi ya kutosha  ambapo kwa sasa uzalishaji ni kidogo sana kwa kile kinachoelezwa kuwa Samaki  aina ya Sangara wamepungua Ziwani na mengine mengi.

Mara baada ya kutembelea Kiwanda hicho Bi. Pendo amepongeza na kushukuru Uongozi wa Kiwanda hicho kwa namna kilivyojizatiti kwa Miundo mbinu katika kuhakikisha kinazalisha bidhaa bora zinazotokana na samaki, na kuongeza kuwa changamoto zote zilizobainishwa, wao kama Washauri katika masuala ya Uwekezaji wanazibeba na watazifikisha katika mamlaka zinazohusika ili zitatuliwe na kuendelea kutengeneza Mazingira mazuri ya mwekezaji huyo kunufaika na uwekezaji wake.

Licha ya changamoto zilizobainishwa na Mwekezaji huyo, Kiwanda Cha Kuchakata minofu ya Samaki cha Supreme Perch kimekuwa kikitengeneza mpaka Bilioni 30 kwa Mwaka kupitia mauzo yao huku Soko la minofu hiyo likiwa Hispania, Italia na Uholanzi, mbali na kutoa ajira kwa Watanzania pia Kiwanda kimekuwa na mchango mkubwa kwa Jamii inayokizunguka kwa kuchangia Shughuli za kimaendeleo ikiwemo Ujenzi wa Visima vya Maji, Shule na wakati mwingine kuwezesha Kliniki inayombetea kwa Wakazi wa Visiwani.


Bi Pendo Gondwe kutoka Kituo Cha Uwezekezaji Tanzania (TIC) akifanya Mazungumzo na Uongozi wa Kiwanda cha Supreme Perch baada ya kuwasili Kiwandani hapo.
Meneja wa Kiwanda Bwana Manoj Manohoran  akiwasilisha changamoto za Kiwanda cha Supreme Perch kwa wawakilishi wa TIC wakati wa Mazungumzo yaliyofanyika Ukumbi wa Mikutano wa Kiwanda hicho.
Eneo mojawapo la mitambo ndani ya Kiwanda ambapo Samaki hupitishwa katika hatua mbalimbali wakati wa uchakataji wa minofu.
Muonekano wa Kifungashio cha Minofu ya Samaki aina ya Sangara inayozalishwa na Kiwanda cha Supreme Perch Bukoba Manispaa.

Maboksi Yenye minofu ya Samaki yakiwa yamefungashwa katika chumba maalum cha kuhifadhia bidhaa hiyo,  tayari kusafirishwa kwenda Sokoni.
Bi. Pendo Gondwe akifurahia pamoja na wenzake Muonekano wa kifungashio cha Minofu ya Samaki cha Supreme Perch.
 Muonekano wa Jengo mojawapo la Kiwanda cha Supreme Perch kilichopo Bukoba Manispaa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...