Na Jusline Marco-Arusha

Wizara ya Katiba na Sheria imefanikisha maboresho ya mfumo wa haki jinai ambayo yatasaidia kutoa muongozo kwa vyombo vyote vya utoaji haki ili uweze kutoa haki kwa wakati kwa watu wote wakiwemo watoto walio katika upinzani wa sheria na waliokutana na sheria.

Akizungumza katika kikao cha kwanza cha Jukwaa la Haki Mtoto,kikao kilichofanyika jijini Arusha Bi.Emma Pastori Lyimo Mkurugezni wa utawala na rasilimali watu kutoka ofisi na wizara ya katiba na sheria kwa niaba ya mwenyekiti wa Jukwaa hilo ambaye pia ni Katibu Mkuu Wizara ya Katiba ma Sheria Prf.Sifuni Mchome alisema licha ya changamoyo zolizokuwepo katika mkakatibwa awali wa utekelezaji kumekuwapo na mafanikio makubwa ambayo yanapaswa kutunzwaili kuendelea kulindwa na kuhifadhi haki ya mtoto kwa maendeleo endelevu.

"Sisi sote ni wadau muhimu katika kuhakikisha kuwa masuala ya haki mtoto yanasimamiwabkwa uweledi."Alisema

Alisema ni vyema changamoto zolizopo kutumiwa kama fursa ya za kipanga na kutekeleza zumuni la lengo lolilokusudiwa kwani watoto ndiyo kiini cha taifa lolote na oli taifa liendelee kuwepo ni lazima watoto waweze kuwepo.

Alirleza kuwa Serikali chini ya utaratibu wa ofisi ya waziri mkuu iliandaa mpango kazi wa taifa wa kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto kuanzia ngazi ya taifa hadi kijiji kwa lengo la kuyalinda makundi maalumu ndani ya jamii dhidi ya vitendo vya ukatili ambavyo vimekuwa vikifanya dhidi yao.

Vilevile aliwataka wajumbe hao kuongeza nguvu na rasilimali nyingi zaidi katika katika kulinda haki za mtoto kwa ajili ya uhai,ustawi,ulinzi na usalama wa tanzania ya leo na hata baadae oli taifa liweze kuwepo.

Aidha aliongeza kuwa katika utekelezaji wa mkakati wa kwanza wa miaka 5 ambao ulikuwa mwaka 2013/2017 ambapo amesema kwa ushirikiano wa pamoja wataweza kuona utekelezaji wa mkakati wa 2021 hadi 2425 wakiuwianisha na mkakati wa awali na malengo yaliyokusudiwa katika makakati wa pili amabayo yataboresha mkakati wa awali kwa ajili ya kumtetea mtoto.

Kwa upande wake wakili wa serikali kutoka ofisi ya Taifa ya mashtaka Beatrece Mpembo kwa niaba ya washiriki wenzake katika kikao hicho aliishukuru wizara ya katiba na sheria kwa kuwaamini na kuweza kuwakutanisha tena kwa ajili ya utekelezaji wa mkakati wa pili baada ya mkakati wa kwanza kumalizika.

Alisema kuwa mkakati wa pili umetoa dira ya kuonyesha mafanikio ambayo waliyapata kipitia mkakati wa kwanza,na kuwaonyesha mapungufu ambayo waliyapata kupitia utekelezaji wa mkakati wa kwanza ambapo mkakati huo pia unatoa uelekeo wa nini kifanyike na kukamilisha kupitia taasisi husika.

"Kwa niaba ya washiriki wenzangu tunauzoefu na kwakuwa mmetuamini tena kuwa mabalozi wa kuziwakilisha taasisi zetu kwaajili ya kuja kutekeleza mkakati wa pili wa 'haki mtoto'tunaahidi uzoefu ambao tuliupata kupitia utekelezaji wa mkakati wa kwanza tutautumia ile na kuongeza vingine vizuri zaidi".Alisema Beatrece

Aliongeza kuwa watatumia changamoto walizozipata katika mkakati wa kwanza kama fursa ili kuweza kutekeleza mkakati wa pili kwa kiwango cha asilimia 100.


 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...