Katibu
Mkuu wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Hassan Abbasi
amewaasa Wafanyakazi wa Kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN) kufanya
kazi kwa weledi ili kupata mafanikio zaidi katika Kampuni hiyo na nchi.
Dkt.
Abbasi ameyasema hayo Mei 4, 2021 alipofanya ziara kwenye Kampuni hiyo
kukagua utendaji wa kazi na kujadiliana na Menejimenti na Wafanyakazi
namna bora ya kuongeza ufanisi wa kazi.
Amesema
TSN ni Kampuni ya Serikali inayoaminika hivyo watumishi wanapaswa
kufanya kazi kwa weledi ili kuendelea kutoa taarifa zenye ubora
zinazozingatia Misingi ya Taaluma ya Uandishi wa Habari.
Amewashukuru
wafanyakazi hao kwa kuendelea kutoa ushirikiano kabla na baada ya
kuteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu
Hassan kushika tena wadhifa huo hivi karibuni.
“Asanteni
kwa ushirikiano mliouonesha kwangu kipindi nina kofia ya Msemaji Mkuu
wa Serikali hadi sasa nimeenda kuwa Katibu Mkuu, hamkuchoka na tulifanya
kazi usiku na mchana, tuendelee kushirikiana bila kuchoka, ili kukidhi
matarajio ya Rais wetu na wananchi kwa ujumla” amesisitiza Dkt. Abbasi.
Akiwa katika ziara hiyo, pia ameitaka Menejimenti ya TSN kujali maslahi ya wafanyakazi wote ili kuleta ufanisi wenye tija.
Naye
Kaimu Mhariri Mtendaji wa Kampuni hiyo Bibi. Tuma Abdallah amempongeza
Katibu Mkuu huyo kwa kuaminiwa tena katika nafasi hiyo na kuahidi kumpa
ushirikiano katika kutekeleza majukumu yake.
Hii
ni ziara ya kwanza ya kikazi aliyoifanya Katibu Mkuu, Dkt. Abbasi
mara baada ya kuteuliwa tena hivi karibuni na Rais wa Jamhuri ya
Muungano Mhe. Samia Suluhu Hassan kushika nafasi hiyo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...