Katibu Tawala wa Mkoa wa mkoa wa Dar es Salaam na mwenyekiti wa kamati ya Maafa ya kimkoa, Paulo Mshimo Makanza  amefunga mradi wa Jipange(Jipange Project) uliokuwa na lengo la kutoa mafunzo kwa
kwa kata 12 zilizopo katika Manispaa ya Kinondoni na Jiji la Ilala.
 
Akizungumza kwenye mkutano huo Katibu tawala Makanza ameushukuru uongozi wa mradi wa Jipange(Jipange Project) kwa kutoa elimu ya namna ya kujiandaa kwenye  kujikinga na maafa kabla ya kutokea ambayo imenufaisha kata zipatazo 12 za  Manispaa ya Kinondoni na Jiji la Ilala.
 
Kata zilizonufaika na mradi wa Jipange ni  kata nane za manispaa ya Kinondoni ambazo ni Kigogo, Tandale, Kawe, Mzimuni, Mwananyamala, Magomeni, Ndugumbi and Mbweni pamoja na  kata 4 za Jiji la Ilala ambazo ni Jangwani, Vingunguti, Mchikichini and Mnyamani.
Mgeni rasmi Katibu Tawala wa Mkoa wa mkoa wa Dar es Salaam na mwenyekiti wa kamati ya Maafa ya kimkoa, Paulo Mshimo Makanza akizungumza na wajumbe wa kamati za maafa wa Manispaa ya Kinondoni na Jiji la Ilala wakati wa kufunga programu ya mafunzi kwa kata 12 kuhusu namna ya kujiandaa na maafa na namna ya kukabiliana na maafa hayo katika jamii.
Meneja wa Mradi wa Jipange  Shamim Zakaria akiwasilisha mada kwa wajumbe wa kamati za maafa wa Manispaa ya Kinondoni na Jiji la Ilala  kuhusu namna walivyoweza kufanikisha utoaji wa elimu kwenye kata 12kuhusu namna ya kujikinga na maafa kabla ya kutokea na baada ya kutokea kupitia mradi wa Jipange(Jipange Project) pamoja na kutoa mipango mikakati ya uratibu wa Maafa kwa wajumbe hao.
  Ofisa kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu - Idara ya Uratibu wa Maafa, Charles Msangi akitoa mada kuhusu sheria za usimamizi wa maafa katika ngazi za kijiji mpaka kitaifa wakati wa ufungaji wa mradi wa Jipange kwa kwa wajumbe wa kamati za maafa wa Manispaa ya Kinondoni na Jiji la Ilala.
Mgeni rasmi Katibu Tawala wa Mkoa wa mkoa wa Dar es Salaam na mwenyekiti wa kamati ya Maafa ya kimkoa, Paulo Mshimo Makanza(wa tatu kushoto) akiwakabidhi mipango mikakati ya uratibu wa maafa kwa baadhi ya wajumbe wa kata wa kamati za maafa wa Manispaa ya Kinondoni na Jiji la Ilala wakati wa kufunga mradi wa Jipange
Mgeni rasmi Katibu Tawala wa Mkoa wa mkoa wa Dar es Salaam na mwenyekiti wa kamati ya Maafa ya kimkoa, Paulo Mshimo Makanza(wa tatu kushoto) akiwakabidhi vifaa vya huduma ya kwanza baadhi ya wajumbe wa kata wa kamati za maafa wa Manispaa ya Kinondoni na Jiji la Ilala wakati wa kufunga mradi wa Jipange
Baadhi ya wajumbe wa  kamati za maafa wa Manispaa ya Kinondoni na Jiji la Ilala wakifuatilia mada zilizokuwa zikitolewa wakati wa kufunga mradi wa Jipange.
Mratibu wa Maafa wa manispaa ya  Kinondoni, Pendo Fredy akitoa shukrani kwa mgeni rasmi pamoja na viongozi wa mradi wa Jipange uliowezesha mafunzo ya kwa kata 12 kuhusu namna ya kujikinga na maafa kabla ya kutokea na baada ya kutokea kwa wajumbe wa  kamati za maafa wa Manispaa ya Kinondoni na Jiji la Ilala.
Mgeni rasmi Katibu Tawala wa Mkoa wa mkoa wa Dar es Salaam na mwenyekiti wa kamati ya Maafa ya kimkoa, Paulo Mshimo Makanza(wa tatu kushoto) akiwa kwenye picha za pamoja na Baadhi ya wajumbe wa  kamati za maafa wa Manispaa ya Kinondoni na Jiji la Ilala pamoja na viongozi wa mradi wa Jipange( Jipange Project)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...