Mkuu wa kitengo Cha Masoko na Uhusiano kwa Umma wa PSPTB, Shamim Mdee 
 
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam 

KATIKA kuhitimisha wiki ya Utumishi wa Umma siku ya Jumatano tarehe 23 Juni, 2021, Bodi ya Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB) imejipanga kutoa mafunzo kwa kundi maalumu la Wanahabari Wanawake wa Dar es Salaam.

Mafunzo hayo yanalengo la kuwajengea uwezo Wanahabari hao juu ya masuala mbalimbali ya fani ya Ununuzi na Ugavi yatakayofanyika katika ukumbi wa PSSSF Golden Jubilee Tower jijini Dar es salaam.

Akizungumza na Michuzi Blog kwa niaba ya Uongozi wa PSPTB, Mkuu wa kitengo Cha Masoko na Uhusiano kwa Umma, Bi Shamim Mdee amesema kuwa milango ipo wazi kwa Watu, Mshirika, Wazabuni au Taasisi mbalimbali kupata ushauri wa kitaaluma katika Bodi hiyo, kwani ni moja ya majukumu yao.

Amesema mafunzo kama haya yamekuwa yakitolewa kwa Taasisi mbalimbali za Umma na binafsi suala ambalo limesaidia taasisi nyingi za umma kupata hati Safi na kupunguza kama sio kuondoka kabisa baadhi ya changamoto zilizokuwa zinawakabili.

“Hali hii itasaidia Wanahabari kubobea katika kuandika na kuripoti kwa ufanisi habari za Ununuzi na Ugavi”, amesema Shamim.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...