Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam 

Katika kipindi cha miezi miwili Shirika la Viwango Tanzania (TBS),limefanikiwa kukusanya shilingi Bilioni 1.9 kutokana na ukaguzi wa magari yanayotoka nje.

Ameyasema hayo leo Meneja wa Ukaguzi wa Bidhaa zinazotoka nje ya nchi (TBS), Mhandisi Saidi Mkwawa katika ofisi za Shirika hilo Jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari Mhandisi Mkwawa amesema kuna umuhimu wa waagizaji wa magari kutumia makampuni kuagiza magari ili kuweza kuepuka kupata hasara kama gari litafika halijakidhi viwango.

Aidha amesema kuwa hapo awali ukaguzi wa magari ulikuwa unafanyika nje ya nchi, Serikali ilikuwa inapata asilimia 30% ya mapato ya ukaguzi ambayo ni sawasawa na Milioni 576.6.

"Hadi sasa ndani ya miezi miwili tumeokoa kiasi cha Bilioni 1.3 ambacho kama magari haya yangekaguliwa nje ya nchi basi fedha hizo zingekuwa katika nchi ambazo zinafanya ukaguzi". Amesema Mhandisi Mkwawa.
Meneja wa Ukaguzi wa Bidhaa zinazotoka nje ya nchi TBS, Mhandisi Saidi Mkwawa akizungumza na waandishi wa habari Makao Makuu ya Shirika hilo leo Jijini Dar es Salaam.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...