Na Mwamvua Mwinyi,Kibaha
Diwani
wa Viti Maalumu Kibaha Mjini ,Lidya Mgaya amesema chanjo ya UVIKO 19
ni mapambano tosha ya kudhibiti ugonjwa huo ikiwa ni pamoja na kujikinga
kwa barakoa na kunawa maji tiririka.
Ametoa
pongezi kwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania baada ya kuzindua hatua ya Kisayansi ya kupambana na homa kali
ya Mapafu UVIKO 19 kwa kutumia njia ya Chanjo.
Lydia alieleza hayo mara baada ya yeye kupata Chanjo ya UVIKO-19 leo Kibaha Mjini.
Lydia
ameeleza kuwa Pamoja na chanjo hiyo kuwekwa katika Hiari ya Mtu lakini
ni vema watanzania kujitokeza kuunga juhudi hiyo ya kisayansi kwani
yeye binafsi akiwa kama mama wa watoto wanne ambao wote aliwapatia
chanjo za kupambambana na maradhi mbalimbali nakuona faida yake, hivyo
atakuwa mstari wa Mbele kujitokeza kwenda kuchanja ili kuendeleza
Mapambano ya UVIKO-19.
“
Nimefurahi sana Kupata chanjo ya UVIKO-19 hapa Kibaha Mjini Baaada ya
Kupewa Taarifa na Mwenyekiti wangu wa UWT Wa Mkoa wa Pwani, nimefurahi
sana kupokea Chanjo nikiwa na Mume wangu ambaye yeye atapokea Chanjo
katika Kituo Cha Lugalo Kesho” alisema Lydia
Aidha
Lydia amempongeza , Rais Samia kwa kuongoza kwa vitendo kwa yeye
binafsi Kuchanja ikiwa ni kuonyesha watanzania kuwa sasa tunatumia
silaha nyingine ya Mapambano ya UVIKO-19 ya kisayansi ili kuendelea
kupambana na Homa hiyo kali ya Mapafu.
Anawashauri
watanzania kutumia uhiari wao katika kufanya maamuzi sahihi katika
hatua hii ya kisayansi iliyoanzishwa ya kupambana na UVIKO-19 ili jamii
yetu ya Tanzania iendelee kubaki Salama Zaidi.
*Corona Inazuilika Jikinge Uwakinge Wengine*
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...