Hayo yamesemwa leo tarehe 17 Septemba, 2021 na Katibu wa Halmashuri Kuu ya CCM Taifa Itikadi na Uenezi Ndugu Shaka Hamdu Shaka akiwa Wilayani Mtwara ikiwa ni muendelezo wa ziara ya wajumbe wa sekretariet inayoongozwa na Katibu Mkuu Ndugu Daniel Chongolo.

Wananchi hawana matarajio mengine kwa serikali zaidi ya yale waliyotuchagua nayo ambayo tuliwaahidi wakati wa uchaguzi mkuu kupitia ilani ya CCM ya uchaguzi ya mwaka 2020-2025 hivyo ni lazima sisi tuliopewa dhamana tukaachana na urasimu na maslahi binafsi katika kutekeleza majukumu yetu.

Napenda kuwakumbusha viongozi na watendaji kuwa dhamana walizonazo kwenye ofisi za umma ndani ya serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na CCM chini ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan wananchi wanahitaji maji, ajira, mazingira rafiki ya kibiashara, huduma bora za afya na heshima wanapofika kwenye ofisi za umma kupata huduma. 

Haya yakikosekana wananchi hawatatuelewa. Hivyo ni lazima sisi kama chama tutafuatilia na kuisimamia serikali ili kuhakikisha haya yanatekelezwa kwani tuliyaahidi na moja ya sifa kuu ya chama chetu ni kuahidi na kutekeleza.

Hospitali hii ya kanda ya Mtwara mbali na kuwa ni utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020-2025 pia ni utekelezaji wa azimio la kikao cha halmashauri kuu ya CCM Taifa kilichofanyika Mtwara mwaka 1987 lililotaka ujenzi huo kufanyika.

"Ujenzi wa hospital hii ya kanda Mtwara unagharimu takribani bilioni 15, kukamilika kwake kutawasaidia wananchi wa mikoa hii ya kusini ikiwemo Mtwara kuepuka kusafiri umbali mrefu kufuata huduma za kibingwa katika hospitali ya Taifa Muhimbili pamoja na gharama za muda na fedha.

Pamoja na kasi nzuri ya ujenzi inayofanywa na mkandarasi ambaye ni shirika la Nyumba la Taifa, wizara ya afya imekuwa kikwazo kikubwa katika kuhakikisha hospital hii inakamilika na kuanza kutoa huduma kwa wananchi. Hawajamlipa mkandarasi hati za makipo takribani 4 ambazo ziliwasilishwa muda mrefu."

Shaka ameitaka Wizara ya Afya kuacha sinema za maonesho kwa kutoa maelekezo na ahadi zisizotoa matokeo yanayopimika na kuonekana kwa wananchi.

"Naitaka wizara ya Afya kueleza kama walimdanganya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt Philip Mpango alipofika kuweka jiwe la msingi kwamba mapema mwezi Oktoba hospital hii itakuwa imeanza kutoa huduma lakini ajabu mpaka leo hakuna dalili hizo. Sasa ni vizuri wabadilike waanze kuwa watendaji badala wapiga maneno matupu." Alisisistiza Shaka.

Malengo na mwelekeo wa ilani yetu ya uchaguzi na serikali ni kuboresha ustawi wa wananchi nchini na Rais Samia hatasita kufanya mabadiliko ndani ya serikali ikiwa huduma kwa wananchi zitaonekana kulegalega.

Ikiwa tutashirikiana na kwenda pamoja kwa kufanya kazi kwa bidii, uzalendo na uadilifu mkubwa nchi yetu itafika mbali katika kupata maendeleo endelevu. Hivyo natoa rai kwa wananchi kuipa ushirikiano serikali inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan ili Kazi Iendelee.






 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...