Mwenyekiti wa Kamati ya Taifa ya Huduma kwa Jamii, Jaji Mohammed Gwae (wapili kulia), Katibu wa Kamati ya Taifa ya Huduma kwa Jamii, Aloyce Musika (kulia) pamoja na Wajumbe wa Kamati hiyo wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kumaliza Kikao cha Kamati hiyo kilichofanyika Jijini Dodoma leo.

Baadhi ya Wajumbe wa Kamati ya Taifa ya Huduma kwa Jamii wakiwa katika Kikao cha Kamati hiyo, kilichofanyika leo Septemba 10, 2021, jijini Dodoma.
Mkurugenzi wa Idara ya Huduma za Uangalizi, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Aloyce Musika, ambaye ni Katibu wa Kamati ya Taifa ya Huduma kwa Jamii, akiwasilisha Taarifa ya Utekelezaji wa Majukumu ya Idara ya Huduma za Uangalizi katika Kikao cha Kamati hiyo, kilichoifanyika, jijini Dodoma, leo.Katibu huyo alisema kuwa katika kipindi cha kuanzia Julai 2020 hadi kufikia Julai 2021, Idara imefanikiwa kuwasajili Wafungwa 3496 na kuwawezesha kutumikia adhabu nje ya magereza hivyo kupunguza msongamano magerezani.
 

Mwenyekiti wa Kamati ya Taifa ya Huduma kwa Jamii, Jaji Mohammed Gwae, akizungumza katika Kikao cha Kamati ya Taifa ya Huduma kwa Jamii baada ya kutambulishwa kwa Wajumbe kuwa Mwenyekiti mpya wa Kamati hiyo. Kikao hicho kilifanyika leo Septemba 10, 2021, jijini Dodoma. Mwenyekiti huyo aliwaambia Wajumbe wa Kamati hiyo kuwa ni wajibu wao kufuata sheria na kumshauri Mhe. Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...