Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi CCM Ndg. Daniel Chongolo amewataka Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA), kuchangamka kununua mahindi kwa wakati ili kuwafanya wakulima kuendelea na shughuli zao za maendeleo.

Katibu Mkuu ameyasema hayo Ruvuma wilayani Mbinga wakati akiongea na wananchi na wanachama wa Chama hicho wakati wa ziara ya wajumbe wa  Sekretariet ya Halmashauri kuu ya CCM Taifa.

Ambapo  amesema, tayari Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan ametoa fedha shilingi bilioni 50 kwa ajili ya Ununuzi wa mahindi hayo kwa wakulima kwa awamu ya pili.

Katibu Mkuu amesema, Rais Samia ametoa fedha za kununulia mahindi ni lazima watu wa NFRA waweze kuchangamka  kwani kazi ya fedha sio kukaa katika mifuko au akaunti za Taasisi, kazi yake ni kuelekea kwenye maeneo  yaliyokusudiwa.

"Mwananchi amelima shamba lake kwa bidii, kavuna vizuri mazao yake  anataka  kutengeneza mambo yake na anataka kujipanga na pembejeo za msimu ujao  wakicheleweshwa kwenye mambo ya Msingi watakuwa hawatendewi haki." Katibu Mkuu

"Sisi tufanye kazi yetu ya singi tununue mahindi kwa wakati,mahindi yakishanunuliwa Mwananchi  atajipangia mwenyewe manunuzi yake kwa sababu fedha ni ya kwake mwenyewe," Katibu Mkuu amesisitiza

Katika hatua nyingine, Katibu Mkuu amewaomba wananchi wa Mbinga kulima mazao mengine ambayo yanastahimili  kwenye eneo la mkoa huo ili kuendeleza kupanua wigo wa mzunguko wa kipato.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...