Raisa Said,Handeni.


Mwenyekiti wa Handeni Mji mkoani Tanga Mussa Mkombati amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu kwa kuwapelekea fedha nyingi katika Miradi ya maendeleo iliyopo ndani ya mji huo.

Akizungumza  wakati wa uzinduzi wa Samia Cup alisema kuwa kitendo cha kuanzisha ligi hiyo nikurudisha fadhira kwa Kiongozi wa nchi aliyewasaidia katika Miradi ya maendeleo .

Mkombati alisema Serikali ya Awamu ya sita inafanya kazi  kubwa katika suala zima la kusukuma maendeleo katika jamii jambo ambalo alieleza ni lazima waiunge mkono ili izidi kuwaletea bajeti kubwa katika Miradi hiyo.

" Sisi watu wa Handeni Changamoto yetu kubwa ni maji lakini  tangu Serikali ya Awamu ya sita iingie madarakani tumepewa visima 15 vyenye thamani ya sh .Milion 345 na mradi mkubwa wa maji kata ya malezi wenye thamani ya Milion 248" Alisema Mwenyekiti huyo

 Alisema kuwa mbali na kupata visima lakini pia wamepewa mradi mkubwa wa bwawa la Kwenkambala  lenye ukubwa wa viwanja vitatu vya mpira lenye thamani ya sh billion 1.96  na pia ukarabati wa bwawa la chanika ambalo linasaidia  kwasasa kutoa maji ambao unaendelea  wanaamini miradi hiyo itakapokamilika itasaidia kupunguza changamoto hiyo ya muda mrefu.

Mkombati alieleza pia Kuna mradi mkubwa wa maji wa miji 28 wenye thamani ya bilion 380 mji wa handeni ni Mmoja wapo  nakwamba endapo miradi yote ikikamilika itakamilisha ndoto ya Rais ya kumtua mama ndo kichwani  hivyo mji handeni utakwenda kupata maji safi na salama.

Mwenyekiti huyo alisisitiza kuwa wakati wa majumuisho ya ziara ya Waziri wa Maji  hivi karibuni katika kata ya mabanda,Waziri aliahidi kutoa Milion 671 ili zisaidie kutoa maji konje kupeleka mabanda na zitasaidia kununua pampu za maji ili zisaidie kukarabati  mradi wa HTM uliopo.

Awali akizindua ligi hiyo itayozikutanisha kata zote 12  za mji huo na mitaa yote 60 ,Mbunge wa Jimbo hilo Ruben Kwagwilwa Alisema kuwa lengo la kuanzisha  mashindano hayo ni kutaka  kufikisha Asante kwa Rais kwa kuwapatia upendeleo wa kuwapa Miradi mikubwa na ya kipekee katika mji wao.

Kwagilwa Alisema kuwa tangu dunia iumbwe mji wa handeni haujawahi kuwa na taa za barabarani lakini kipindi hiki inawaka.

Hata hivyo Mbunge huyo Alisema licha ya kufikisha Asante kwa Rais kupitia ligi hiyo  lakini pia ni sehemu ya utekelezaji wa ilani na ahadi alizozitoa wakati akipita kuomba kura kipindi cha kampeni.



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...