*Kiwanda kilenge ubora wa kimataifa

*KASHIMBA: Watanzania wanapatiwa ujuzi na wataalam wa kigeni

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria imewataka wawekezaji na wafanyakazi wa kiwanda cha kimataifa cha bidhaa za ngozi Kilimanjaro (KLICL) kufanyakazi kwa juhudi, weledi na maarifa ili makusudio ya kuanzishwa kwa kiwanda yafikiwe.

Hayo yalisemwa Oktoba 23, 2021 na  Kaimu Mwenyekiti wa kamati hiyo, Mhe. Najma Murtaza Giga wakati wa ziara ya kamati ya kudumu ya Bunge katika kiwanda cha bidhaa za ngozi cha Kilimanjaro, kilichopo mjini Moshi mkoani Kilimanjaro.

“kamati itaendelea kusimamia na kushauri ili kiwanda kiwe endelevu kwa maslahi ya wananchi kwa ujumla” alisisitiza Mhe. Giga.

Mhe. Giga aliwataka watumishi wa kiwanda kuwa wabunifu na waaminifu katika kulinda miundombinu ya kiwanda ambacho ni mali ya watanzania wote.

Kwa ujumla wajumbe kamati wamepongeza mipango ya kiwanda hicho na kushauri kilenge kuwa na viwango vya kimataifa, pia pongezi ilitolewa kwa kutoa ajira kwa watanzania wengi ikiwemo vijana na wanawake. kamati  ilishauri elimu zaidi itolewe juu ya bidhaa za kiwanda hicho na maduka yasambae nchi nzima.

Kwa upande wake mjumbe wa kamati hiyo na Mbunge wa jimbo la Chonge, Mhe. Salum Saffi alishauri kiwanda hicho kujipanga kuwa na wataalam wazawa na kuachana na tabia ya kutegemea wageni katika uendeshaji wake.

Naye Mhe. Omary Omary alisema, “Kwa upande wangu nimeshaanza kutumia bidhaa za kiwanda hiki, naomba kiwanda  kilengi kuzalisha bidhaa bora za viwango ili kiweze kupata soko la uhakika, haswa kwa soko la Zanzibar”.

Mbuge wa Moshi Mjini, Mhe. Priscus Tarimo alisema, “Wana Moshi wapo tayari kulinda kiwanda hili. Pia nashauri ili tuweze kupata soko la uhakika la bidhaa za kiwanda hiki, tuhakikishe bidhaa zilizo chini ya viwango haziruhusiwi kuigizwa nchini,”.

Kwa upande wake, Naibu Waziri ofisi ya Waziri Mkuu anayeshugulikia Kazi, Vijana na Ajira Bw. Patrobas Katambi alishukuru kamati hiyo kwa kutembelea kiwanda na kusema hoja zote zimepokelewa na zitafanyiwa kazi vyema.

Naye Mwenyekiti wa Bodi ya Kiwanda hicho, CPA. Hosea kashimba alisema wataalam kutoka nje waliopo kiwanda wanatoa elimu kwa watumishi watanzania kwa kila hatua ili waweze kuendesha vilivyo kiwanda wakati wote.

“Wataalam waliopo kiwanda wanafunga mashine mbalimbali, tumekubaliana watumishi wa kitanzania wahusike katika kila hatua ili waweze kupata ujuzi na hatimaye kiwanda tukiendeshe wenyewe” alisema Mwenyekiti huyo ambaye pia ni Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa watumishi wa Umma (PSSSF).

Nae Mkurugenzi Mtendaji wa Kiwanda, Mhandisi Masud Omari alisema kiwanda kimeanza uzalishaji wa bidhaa mbalimbali za ngozi kama; viatu vya kike na kiume, viatu vya shule na viatu vya majeshi yote nchini.

“Tumeaza uzalishaji, hivyo tunatoa wito kwa watanzania wote kuvaa viatu vya kiwanda chetu, kwani ni bora na imara na vinapatikana kwa bei nafuu” alisisitiza Mhandisi Omari.

Kiwanda cha bidhaa za ngozi kinamilikiwa kwa ubia kati ya Jeshi la Magereza na PSSSF.


Naibu Waziri ofisi ya Waziri Mkuu anayeshugulikia Kazi, Vijana na Ajira Bw. Patrobas Katambi (wakwanza Julia), Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Profesa Jamal Katundu (wakwanza kushoto), Mwenyekiti wa Bodi ya Kiwanda cha Kimataifa cha Bidhaa za Ngozi Kilimanjaro (KLICL) ambaye pia ni Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma,(PSSSF) C.P.A Hosea Kashimba (wapili kushoto) na Mkurugenzi Mtendaji wa Kiwanda, Mhandisi Masud Omari  wakiangalia viatu vinavyotegenezwa katika  Kiwanda hicho wakati wa ziara ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria, mjini Moshi.
Kaimu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria, Mhe. Najma Murtaza Giga (kushoto aliyevaa hijab) akiangalia viatu vinavyotegenezwa KLICL
Kaimu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria, Mhe. Najma Murtaza Giga (aliyevaa hijab) akiteta jambo na C.P.A Kashimba wakati yeye na wajumbe wa Kamati yake walipotembelea Kiwanda hicho. Wakwanza kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe.Stephene Kagaigai.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kiwanda, Mhandisi Masud Omari akizungumza.
Naibu Waziri ofisi ya Waziri Mkuu anayeshugulikia Kazi, Vijana na Ajira Bw. Patrobas Katambi akizungumza.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Mhe. Stephen Kagaigai akiangalia moja ya viatu vinavyotegenezwa na kiwanda Cha KLICL
Mkurugenzi Mtendaji wa Kiwanda, Mhandisi Masud Omari (kushoto), akitoa maelezo kwa Mhe. Katàmbi, Mwenyekiti wa Kamati Mhe. Giga na wajumbe kuhusu shughuli za Kiwanda.
Wajumbe wa Kamati wakiwa kiwandani


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...