Na Khadija Kalili, Kibaha
Serikali Mkoa wa pwani imesaini  mkataba wa kazi za  ujenzi za barabara za  TARURA na  Kampuni 17  huku kiasi  cha  Bil.43.3 zimetengwa kwa ajili ya ujenzi huo wa barabara  ikiwa ni ongezeko la bajeti  mara 4 ya bajeti  ya mwaka wa fedha 20/21.

Akizungumza Wilayani Kibaha Mkoani Pwani wakati akishuhudia hafla ya utiaji saini wa mkataba huo  uliyofanyika kati ya  TARURA na makampuni 17  yaliyoshinda zabuni hiyo.
 Mkuu wa Mkoa wa Pwani  Alhaj Abubakari  Kunenge ameagiza fedha hizo kusimamiwa vizuri pamoja na kuwataka wakandarasi kumaliza kazi kwa wakati uliopangwa.
 
Akisoma taarifa ya TARURA   Meneja wa TARURA  Mkoa wa  Pwani  Mhandisi Leopold Runji amesema mkataba huo unaenda kurahisisha  upatikanaji wa huduma za kijamii  na mawasiliano na kukuza uchumi wa  Mkoa wa Pwani na taifa kwa ujumla.

Naye Mhandisi Angela  Shayo  Akizungumza kwa niaba ya Wahandisi  wengine kutoka Kampuni ya  Isimila  Limited alisema  kuwa wao kama wakandarasi watahakikisha wanakamilisha kazi kwa wakati  na kutimiza wito wa kwenda na wakati kama jinsi walivyoelekekezwa na RC Kunenge.

Hata hivyo  jumla ya Bil 6.3 zimesainiwa ambapo TARURA Mkoa wa Pwani wamepokea kiasi cha shilingi  Bil.2.3 kwa ajili ya ujenzi na matengenezo ya miundo mbinu ya barabara za  Mkoa wa Pwani ambapo bajeti hiyo kwa TARURA  inaenda kuongeza urefu wa barabara kutoka urefu wa KLM 57 za sasa mpaka KLM 74 sawa na ongezeko la KM 17 ambalo ni zaidi ya asilimia 29 mwaka wa fedha 21/22.
Wakati huohuo RC Kunenge amewaagiza wakandarasi hao kuhakikisha wanasimamia ujenzi wa barabara  hizo na kuzikamilisha kwa wakati  muafaka.

"Kamilisheni  barabara hizi kwa wakati  mliopewa  Mimi kama Kiongozi  wenu katika  ngazi ya Mkoa nawaheshimu  kilammoja  kwa fani yake hivyo nawaaahidi kuwa nitakuwa nafanya ziara za kushtukiza katika maneno yenu ya kazi ili kuona namna kazi zinavyofanyika hata kama itakua ni usiku wa manane nitapita kuwakagua " alisema RC Kunenge.

Aidha aliongeza kwa kuwaasa wakandarasi hao kuwa ni marufuku kutoa fedha kwa mtu yeyote yule hata kama atasema  kuwa wametumwa na RC kumbukeni  kuwa mafanikio  ya kupata fedha  hizi za miradi imetokana na juhudi zenu  binafsi na siyo vinginevyo  nasema haya na Taasisi ya Kuzuia na Kupambania na Rushwa wananisikia" alisema RC Kunenge.





Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...