kutoka kulia ni Sajenti Juma Mabeyo ,Mkaguzi
wa magari na msaili wa madereva kutoka mkoa wa Manyara akionyesha
baadhi ya vifaa wanavyotumia kwenye zoezi la ukguzi wa magari
(aliyeshika kioanzasauti)Sajenti Paschal Kimario ,Mkaguzi wa magari na msaili wa madereva kutoka mkoa wa Arusha akitoa ufafanuzi kwa mgeni rasmi Mkuu wa Mkoa John Mongela
wa kwanza kushoto ni Mkaguzi wa magari sanjenti Paschal Kimaro akitoa maelezo juu ya vifaa vya kukaguliwa magari kwa mgeni rasmi ambaye ni mkuu wa mkoa wa Arusha John Mongela,kulia ni Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha ACP Justine Masejo
kutoka kulia ni Sajenti Juma Mabeyo ,Mkaguzi wa magari na msaili wa madereva kutoka mkoa wa Manyara (aliyeshika kioanzasauti)Sajenti Paschal Kimario ,Mkaguzi wa magari na msaili wa madereva kutoka mkoa wa Arusha akitoa ufafanuzi kwa mgeni rasmi Mkuu wa Mkoa John Mongela
Mkuu wa mkoa John Mongela
akiangalia z basi la Abiria ambalo limefanyiwa ukaguzi katika uzinduzi
wa zoezi la ukaguzi wa vyombo vya Moto katika viwanja vya soweto
Jijini Arusha
Mkuu wa mkoa wa Arusha John Mongela akizungumza na wadau wa usafirishaji katika uzinduzi wa ukaguzi wa vyombo vya Moto uliofanyika katika viwanja vya soweto Jijini Arusha
Mkuu wa Usalama barabarani Mkoa wa Arusha Mrakibu wa polisi Solomon Mwangamilo,akizungumza
katika uzinduzi wa ukaguzi wa vyombo vya Moto katika viwanja vya soweto
Jijini Arusha,kulia kwake ni mwenyekiti wa Kamati ya Usalama barabarani
Gelace Rutachubirwa
UZINDUZI WA ZOEZI LA UKAGUZI WA VYOMBO VYA MOTO WAFANYIKA ARUSHA
Na Vero Ignatus,Arusha
Uzinduzi
wa ukaguzi wa vyombo vya Moto imefanyika rasmi Jijini Arusha,ukiwa na
lengo la kutoa Elimu kwa Jamii kuelekea maadhimisho ya wiki ya nenda
kwa usalama barabarani ambayo Kitaifa yatafanyika mkoani Arusha kuanzia
tarehe 15.11.2021 hadi tarehe 20.11.2021.
Mkuu wa Usalama barabarani Mkoa wa Arusha Mrakibu wa Polisi Solomon Mwangamilo ,akitoa taarifa
fupi kuhusiana na maadhimisho hayo alisema lengo ni kutoa nafasi kwa
Baraza la Usalama barabarani ,kufanya tathmini ya jumla kwa mwaka mzima
,kuhusiana na usalama wa watumiaji wa vyombo vya moto, kuangalia maeneo
ambayo yanapelekea ajali nyingi za barabarani na kuja na mikakati ya
kupunguza ajali hizo.
Mwangamilo alisema
wataendelea watatoa elimu ikiwa ni pamoja na kukagua vyombo vyote vya
moto vilivyopo mkoani Arusha, ambapo wametenga maeneo tofauti kwa ajili
ya zoezi hilo kwa kuzingatia ukubwa wa Jiji, zoezi litafanyika katika
vituo vya Polisi, viwanja vya Soweto na kwa upande wa wanaomiliki idadi
kubwa ya vyombo vya moto watapeleka Wakaguzi wa magari kwenda kufanya
ukaguzi katika maeneo yao, baada ya kupokea maombi lengo likiwa ni
kupunguza ucheleweshwaji wa utoaji huduma.
Kwa upande wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha ACP Justine Masejo ,wakati
akimkaribisha Mkuu wa Mkoa alisema kama Watumiaji wa vyombo vya moto
watafuata kauli mbiu ya utii wa Sheria bila shuruti watapunguza ajali nyingi za barabarani ambazo zimepelekea watu wengi kupoteza maisha, ulemavu pamoja na uharibu wa vyombo vya moto.
Akizungumza mgeni rasmi katika uzinduzi wa zoezi hilo, Mkuu wa Mkoa wa Arusha John Mongela, ameanza
kwa kulipongeza Jeshi la polisi kupunguza matukio ya ajali za
barabarani,pamoja na ubunifu wa kwenda katika maeneo ya wanaomiliki
idadi kubwa ya vyombo vya moto ,kwa ajili ya kukagua vyombo vyao.
Mongela alisema
ni muhimu Wananchi waendelee kuelimishwa, kuhusiana na sheria za
usalama barabarani,na kukemea vitendo vya rushwa kwa Askari wachache
ambao wanachafua taswira ya Jeshi la Polisi.
Niwapongeze
wadau wa usalama barabarani, hususani madereva kwa kujitokeza kwa
wingi kwa ajili ya ukaguzi wa vyombo vyao,niliombe Jeshi la polisi kupitia Kitengo Cha Usalama barabarani zoezi hili liwe na ufanisi lisigeuke kuwa kero,na kuzalisha malalamiko.alisema
Jeshi
la polisi ndio msingi wa Dola na mmepewa jukumu la moja kwa moja
kukutana na changamoto za wananchi pamoja na malalamiko
yao,hatuhalalishi kero Ila nasema wakati mwingine,ukindoa wale wachache
,ambao wanaosababisha kero zisizo za msingi ya kutokua na uadilifu
Mongela alisisitiza kuwa kutoa Elimu isiwe kwa wananchi na wadau wa nje pekee, bali hata ndani ya Jeshi la Polisi lenyewe,ili kukumbushana wajibu na viapo vyao,ili kuweza kuwa wasafi zaidi na kuepukana malalamiko na lawama zipungue.
"Wakati
inapobidi tuchukue hatua maana unajua Kuna mtu kazaliwa mtukutu na
kadhapenya Sasa na kila unavyofanya wewe unakuwa Kama unsmchochea,
anafanya zaidi,Sasa hatua zichukuliwe kwasababu mwisho wa siku Jeshi
zima linaonekana Kama linatatizo kumbe ni watu wachache tu"Alisema Mongela
Alimaliza kwa kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan
kwa kuelekeza maadhimisho hayo kitaifa yafanyike Mkoa wa Arusha, hivyo
akatoa wito kwa wadau wa usalama barabarani kushikama na kujitoa kwa
pamoja ili kuhakikisha maadhimisho hayo yanafanyika kwa hali ya amani
na utulivu
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...