NA FARIDA SAIDY,KILOMBERO.

Viongozi wa madhehebu ya dini Mkoani Morogoro wamewataka waumini wa madhehebu yao na watanzania kwa ujumla kuacha tabia ya kulalamikia viongozi wa Serikali badala yake wawape muda wa kutekeleza majukumu yao huku wakiwaunga mkono kwa kufanya kazi za kujiingizia kipato sambamba na ulipaji kodi bila shuruti.

Wito huo umetolewa wilayani Kilombero na Askofu Mkuu wa makanisa ya free pentekoste  Tanzania FPCT Askofu Stivine Mulenga,wakati wa hafla ya kumsimika askofu mpya wa jimbo la kilombero.

 Askofu  Mulenga amesema kuwa ni muda sasa wakuacha kuitupia Serikali lawama badala yake kufanya kazi kwa bidii na kushrikiana na Serikali ili kukuza uchumi wa nchi hali itakayosaidia kubadilisha maisha ya kila moja hapa nchini.

“Ni lazima tuwape muda viongozi wetu,hata ukimuchagua wa chama kingine hawezi kufanya kazi unavyotaka wewe lazima achague upande sahihi”.Alisema askofu Mwanga.

Aidha amewataka waumini kuwaheshimu viongozi wao pamoja na kuwaombea viongozi “kwani neno la mungu linasema lazima tuiombee serikali na viongozi wake” .Alisema Mwanga.

Kwa upande wake Askofu Mstaafu wa Kanisa la Kipentekoste Jimbo la Kilombero Askofu Lameck Bwango naye alikuwa na haya ya kusema

Nao  wamumini na wa kanisa hilo akiwemo Barnabas Bwango na Esther Mkwazu wamewataka vijana kufanya kazi kwa nguvu zao zote ili kuondoa malalamiko ya ugumu wa maisha na ukosefu wa ajira


 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...