Waziri wa Madini,Dk. Doto Biteko akihutubia wajumbe wa mkutano Mkuu wa 24 wa TAWOMA uliodhaminiwa na kampuni ya madini ya Barrick



Katika mwendelezo wake wa kufanya kazi na wadau mbalimbali, kampuni ya madini ya Barrick imedhamini mkutano wa 24 wa Chama cha Wachimbaji Madini Wanawake Tanzania (TAWOMA) mwaka huu uliofanyika mkoani Dodoma na kufunguliwa na Waziri wa Madini, Dk.Doto Biteko.

Mkutano huo ulihusisha na maonesho ya bidhaa za madini kutoka kwa wanachama wa chama hicho ambacho kilianzishwa mwaka 1992 kikiwa na malengo ya ni kuhamasisha Wanawake wengi kuingia kwenye Sekta ya Madini na kuwakomboa kiuchumi kupitia Elimu, Mitaji na Masoko.

Barrick imeeleza kuwa itaendelea kusaidia shughuli mbalimbali kupitia sera ya kusaidia huduma za kijamii ambayo imefanikisha miradi mbalimbali ya kuwakomboa wananchi kiuchumi katika maeneo yanayozunguka migodi yake pia inaendelea kuwezesha miradi ya afya na elimu sambamba na kufadhili progamu za kuwapatia wananchi elimu ya ujasiriamali na kilimo cha kisasa.
Wajumbe wa mkutano mkuu wa TAWOMA wakifuatilia hotuba ya Waziri wa Madini, Dk. Doto Biteko.
Wajumbe wa mkutano mkuu wa TAWOMA wakifuatilia hotuba ya Waziri wa Madini, Dk. Doto Biteko.
Wajumbe wa mkutano mkuu wa TAWOMA wakifuatilia hotuba ya Waziri wa Madini, Dk. Doto Biteko.
Wajumbe wa mkutano mkuu wa TAWOMA wakifuatilia hotuba ya Waziri wa Madini, Dk. Doto Biteko.
Wanachama wa TAWOMA walipata fursa ya kuonyesha shughuli zao

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...