Akitoa salamu za Serikali, Waziri wa Nchi Ofisi ya Raais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Innocent Bashungwa ametoa pole kwa familia kwa msiba huo mzito.Amesema kutokana na wema wa Mhe.Shigela ndio sababu ya watu wengi wamejitokeza kumfatiji kufuatia msiba huo wa mke wake.

"Mhe. Martine  ni mtu mwema mwenye ushirikiano wa hali ya juu tangu nilipokutana naye  nikiwa Wizara ya Viwanda na biashara, Kilimo na hadi leo hii,"amesema

 Mhe. Bashungwa amesema TAMISEMI inatoa pole na kuwashukuru wakuu wote wa Mikoa Tanzania bara kwa ushirikiano walionyesha katika kupindi hiki kigumu cha msiba wa Bi. Magdalena aliyefariki   tarehe 20.01.20211 na hadi anazikwa 

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Innocent Bashungwa akitoa heshima za mwisho kwenye jeneza lililobeba mwili wa  Mke wa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Martine Shigela katika mazishi yaliyofanyika wilayani Kishapu mkoani Shinyanga.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Innocent Bashungwa katikati akiweka shada la maua kwenye kaburi la Mke wa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Martine Shigela yaliyofanyika wilayani Kishapu mkoani Shinyanga.(Pcha zote na Emmanuel Massaka wa Michuzi Tv)











































Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...