Na Mwandishi Wetu Zanzibar
WANAFUNZI 50 wa mwaka wa tatu wa Chuo Kikuu Ardhi (ARU), wako visiwani Zanzibar kwa ajili ya mafunzo ya vitendo kuhusu majengo ya kale.

Akizungumza hivi karibuni, Mhadhiri Msaidizi wa chuo hicho, Richard Moses amesema hiyo ni moja ya sehemu ya ufundishaji wa Chuo inayohusisha kuwanoa wanafunzi kwa njia ya vitendo.

Amesema wanafunzi hao 50 wanaosomea Shahada ya Usanifu Majengo watakaa visiwani humo kwa siku 14 wakijifunza masuala mbalimbali ya usanifu.

Amesema ingawa wanafunzi hao wanasomea usanifu kwa majengo mapya lakini wanalazimika kupata ujuzi kuhusu majengo ya kale kwa kuyapima na kuyarekodi ukubwa wa majengo na yalitumikaje.

“Wanachunguza majengo haya yalipitia matumizi gani mpaka leo hii na pia watapendekeza mabadiliko ambayo yanapaswa kufanywa kwa majengo hayo ili yaendelee kutumika kwa miaka mingi hivyo watajifunza kwa vitendo kuhusu majengo ya kale,” amesema Mhadhiri huyo.

Amesema lengo kubwa hasa la kuwapeleka visiwani Zanzibar ni kuwajengea uwezo wa kuweza kukabiliana na soko la ajira kwa kujua masuala mbalimbali kwa vitendo hivyo kuwaongezea ujuzi.

“Wakiwa hapa Zanzibar wanafunzi hawa wameweza kufanya tathmini katika mji mkongwe maarufu kama ( Stone Town) kwa kupata historia yake, matumizi ya jengo wakati wa zamani na sasa, aina ya ujenzi uliotumika, thamani, na vipimo mbalimbali kwa kuendana na wakati husika,” alisema.

Amesema pamoja na hilo taarifa hizo zinaweza kusaidia kutumika na wataalam mbalimbali hasa kwenye kushauri au kupendekeza juu ya matumizi, thamani na matumizi endelevu ya majengo hayo kongwe kwa manufaa ya vizazi vijavyo.
Wanafunzi wa mwaka wa tatu wa Chuo Kikuu Ardhi (ARU) wakiwa kwenye mafunzo kwa vitendo kisiwani Zanzibar.

Wanafunzi wa mwaka wa tatu wa Chuo Kikuu Ardhi (ARU) wakiendelea na mafunzo yao kwa vitendo visiwani humo ambapo watakaa kwa wiki mbili.
 Wanafunzi wa mwaka wa tatu wa Chuo Kikuu Ardhi (ARU) wakiendelea na mafunzo yao kwa vitendo visiwani humo ambapo watakaa kwa wiki mbili.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...