Na.Abel Paul wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Arusha

Jeshi la Polisi nchini limejipanga vyema kuimarisha ulinzi na usalama baada Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kuzindua filamu ya The Royal Tour hivi karibuni kwa lengo la kuutangaza utalii.

Akitoa taarifa hiyo kwa niaba ya msemaji wa Jeshi la Polisi Nchini, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha Kamishna Msaidizi wa Polisi ACP JUSTINE MASEJO amesema Jeshi la Polisi Nchini limeanzisha kitengo maalumu cha Utalii na Diplomasia ambacho kipo kwa ajili ya kuwahudumia Watalii na Wanadiplomasia wanaofiika nchini.

Aliendelea kusema Mkoa wa Arusha ambapo ni kitovu cha utalii nchini kumeanzishwa kituo cha Polisi maalumu kwa ajili ya kuhudumia Watalii na Wanadiplomasia ambapo Askari wake wamewapatiwa mafunzo ndani na nje ya Nchi namna bora ya kuhudumia watalii.

Pia amesema kuwa kuna magari maalumu ambayo hutumiwa na kituo hicho kwa ajili ya doria mbalimbali ikiwemo kwenye vivutio vya utalii, hoteli za kitalii pamoja na maeneo mengine ambayo wageni hupenda kutembelea.

Sambamba na hilo amesema kuwa kuna vituo vidogo vya Polisi vilivyopo katika wiliya ya Arumeru, Monduli, Longido, na Karatu ambapo magari ya utalii hufika kwa ajili ya kupata taarifa za kitalii pamoja na ukaguzi wa usalama wa magari hayo.

Alimaliza kwa kusema kuwa Jeshi la Polisi Nchini litaendelea kumuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan katika kuutangaza utalii kwa kuboresha mazingira ya kiusalama kwa watalii wanaofika nchini.



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...