Naibu
Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja (Mb) ameongoza ujumbe
wa Tanzania kuhudhuria katika Tamasha la Utalii wa Utamaduni la
kutangaza vyakula vya asili lililoandaliwa na Serikali ya Zimbabwe,
lililofanyika kwenye viwanja vya hoteli ya Elephant Hills katika eneo la
Victoria Falls nchini Zimbabwe.
Akizungumza
baada ya tamasha hilo Mhe. Masanja amesema tamasha hilo ni fursa ya
kipekee ya kutangaza Utalii wa Utamaduni kupitia vyakula vya asili hivyo
Tanzania inaweza kuiga mfano huo wa kutangaza vyakula vya asili ili
kuvutia watalii wengi zaidi.
Mhe.
Masanja ameshiriki katika kutembelea mabanda ya washiriki ambao ni
wazawa wa Zimbabwe, akiwa ameongozana na Mke wa Rais wa Zimbabwe, Dkt.
Amai Auxillia Mnangagwa pamoja na Mawaziri wa Sekta ya Maendeleo ya
Jamii, Mazingira, Maliasili na Utalii kutoka nchi za Zambia, Namibia na
Botswana, na kisha kushiriki katika zoezi la kugawa zawadi kwa washindi
wa mashindano hayo.
Mhe.
Masanja yupo nchini Zimbabwe kwa ajili ya kushiriki kwenye Kongamano la
Tembo wa Afrika litakalofanyika katika Hifadhi ya Taifa Hwange ikiwa na
lengo la kuunda mpango mpya na bora zaidi wa uhifadhi wa Tembo na
kukuza Utalii Barani Afrika.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...