Na. Farida Ramadhan, WFM, Dodoma

Serikali imeeleza kuwa Sheria ya Kudhibiti Utakasishaji wa Fedha Haramu, Ufadhili wa Ugaidi na Ufadhili wa Silaha za Maangamizi haihusiki na utoaji dhamana kwa watuhumiwa wa makosa ya kawaida.

Hayo yameelezwa jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Hamad Hassan Chande alipojibu swali la Mbunge wa Njombe Mjini, Mhe. Deodatus Mwanyika, aliyetaka kujua wakati ambao Serikali itarekebisha Sheria ya Utakasishaji Fedha aliyodai inazuia dhamana kwa watuhumiwa hata kwa makosa ya kawaida.

Mhe. Chande alisema hakuna sababu ya kurekebisha Sheria hiyo kwa kuwa kifungu cha 12 cha Sheria hiyo SURA 423, kinabainisha makosa ya utakasishaji fedha haramu pekee na hakihusiki na masuala ya dhamana kwa makosa ya kawaida.

“Utaratibu wa dhamana kwa makosa mbalimbali, ikiwemo utakasishaji wa fedha haramu unasimamiwa na Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai, SURA 20”, alifafanua Mhe. Chande.

Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Hamad Hassan Chande (Mb)

 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...