Na John Walter-Manyara
Mkoa wa Manyara kwa kushirikiana na Shirika la Afya Ulimwenguni, WHO, kwa pamoja na wadau mbalimbali wameanza kampeni maalum ya kuwachanja wananchi wa mkoa huo dhidi ya COVID-19 kwa kutembea nyumba kwa nyumba ili kuwafikia watu wa jamii zote na walio katika mazingira magumu.

Katika zoezi la kuchanja wananchi dhidi ya ugonjwa huo ambao umepoteza maisha ya wengi na kuwaacha wengi wakiwa yatima na wajane, mkoa wa Manyara unatajwa kushika nafasi ya mwisho kitaifa kuchanja raia wake.
Katibu tawala mkoa wa Manyara Karolina Mthapula amesema wamejipanga kuhakikisha wanafikia lengo.
Hadi sasa mkoa wa Manyara umetoa chanjo kwa watu takribani laki tatu, idadi ambayo ni sawa na asilimia 3.7 tu ya lengo.

Akizungumza mjini Babati wakati wa kikao kazi cha tathmini ya utoaji chanjo ya UVIKO -19, Meneja wa mpango wa chanjo wa Taifa kutoka wizara ya Afya Dkt. Florian Tinuga amesema hadi sasa mkoa wa Ruvuma ndio unaoongoza kitaifa kwa kufikia asilimia 40 ya uchanjaji.

Ikumbukwe kuwa Lengo la kitaifa ni kufikia asilimia 70 ya kutoa chanjo dhidi ya UVIKO -19 ifikapo mwezi Desemba mwaka huu.
Kwa upande wake Mkurugenzi Msaidizi kutoka shirika lisilo la kiserikali la JHPIEGO, Maryrose Giattas amesema shirika lake litatoa zaidi ya shilingi bilioni moja kuunga mkono kampeni ya chanjo dhidi ya UVIKO-19 mkoani Manyara.

Naye mkuu wa mkoa wa Manyara, Makongoro Nyerere amewataka watendaji mkoani humo kuhamasisha wananchi ili wajitokeza na kupata chanjo dhidi ya UVIKO -19.






Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...