Na John Mapepele.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mhe, Samia Suluhu Hassan ametoa vifaa vya michezo kwa timu zote 45 zinazoshiriki mashindano ya kombe la Yamleyamle Zanzibar ili timu ziweze kufanya vizuri hatimaye kuwapata wachezaji bora na wenye vipaji ambao wataunganishwa kwenye timu ya Taifa.

Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo. Mhe, Mohamed Mchengerwa, Julai 3, 2022 wakati akizindua mashindano hayo yanayofanyika kwenye Uwanja wa Amani Zanzibar ambapo amesema Mhe. Rais ametoa mipira 45 kwa ajili ya timu hizo na jezi.

“Niwaombe tunapojipanga kwenda kuandaa mashindano ya AFCON, tuleteeni orodha ya vijana wanaofanya vizuri tutahakikisha tunawaingiza kwenye time zetu za taifa, tutawaendeleza, tutakuza vipaji vyao kwa maslahi ya Serikali zote mbili SMT na SMZ”. Amesisitiza Mhe, Mchengerwa.

Amewapongeza kwa kuandaa mashindano hayo ambapo amefafanua kwamba dhamira ya Serikali ni kuhakikisha kuwa inaandaa mashindano ya AFCON 2027 na kusisitiza kuwa inawezekana iwapo kila mdau atachukua wajibu wake.

Aidha, amefafanua kuwa eneo la soka ndilo eneo pekee ambalo linaweza kuwaunganisha watanzania wote bila kujali itikadi ya dini zao, rangi wala makabila yao.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...