Na Mwamvua Mwinyi,Pwani

KATIBU Tawala Mkoani Pwani (RAS) Mhandisi Mwanasha Tumbo , amewaagiza waratibu na wasimamizi wa fedha za Mfuko wa maendeleo ya jamii (TASAF) ,kupitia mpango wa kunusuru kaya maskini kusimamia na kuhakikisha wanakuwa waadilifu na waaminifu kwa fedha zinazotolewa kwa ajili ya wanufaika .

Ameeleza yapo malalamiko kwa wanufaika Kuwa wakati mwingine fedha hizo haziwafikii Jambo ambalo linachafua mpango mzima wa utekelezaji.

Akifungua kikao kazi cha kujadili shughuli ya mpango kazi wa kunusuru kaya maskini 2021/2022 ,kilichowahusisha wakuu wa idara na vitengo sekretariet ya mkoa na waratibu wa TASAF wa Halmashauri Tisa za mkoa wa Pwani ,Katibu Tawala mkoa huo, Mwanasha Tumbo alisema , malalamiko hayo yanajitokeza kutokana na kuwaachia watendaji na wenyeviti wa vijiji fedha ambapo zinachelewa kuwafikia walengwa.

Alieleza ,jumla ya kaya maskini 29,683 zinanufaika kupitia mpango wa kunusuru kaya maskini Mkoani hapo ambapo sh.Bilioni 5.609,6 zimeshapokelewa kwa mwaka wa fedha 2021/2022 hivyo Lazima zisimamiwe ili kutimiza azma ya Serikali na kujiepusha na migongano.

"Pia Utaratibu wa Sasa mnawatumia fedha kwenye simu ,mitandaoni changamoto iliyopo walengwa wengine hawajui matumizi ya mitandao ya simu ,anamuagiza mjukuu wake ,jirani ama jamaa hadi fedha ikitoka unakuta mlengwa anapata pungufu ama wananufaika ambao hawastahili".

Kutokana na changamoto hiyo ,Mwanasha ameelekeza waangalie namna ya kutoa elimu ya Utaratibu huo ili Hali wahusika wapate Uelewa.

"Fedha hizi tuhakikishe zinawafikia walengwa na kutimiza adhma ya Serikali kusaidia kaya maskini, Mimi mwenyewe Ni shuhuda ,nilifika pale Kimaramisale ,Ni kati ya vijiji vipya vilivyoongezwa ,tumefika pale watu wamepokea fedha zao na wameishukuru Serikali kwani haijawahi kutokea"alifafanua Mwanasha.

Akiwasilisha taarifa ya utekelezaji  mkoa , mratibu wa TASAF Mkoani Pwani Roselyn Kimaro alieleza ,kaya maskini 29,683 zinanufaika na mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF ) kupitia mpango wa kunusuru kaya maskini ambapo Jumla ya sh.Bilioni 5.609,6 zimepokelewa kwa mwaka wa fedha 2021/2022.

Vilevile alifafanua,ipo miradi 168 iliyoibuliwa na wananchi na inaendelea vizuri, yenye thamani ya Bilioni 1.084.

Rosely wamepokea maagizo ya Katibu Tawala mkoa ,na watahakikisha wanasimamia fedha hizo kwa kuimarisha ukaguzi ,na amedai wanaweka mikakati ya kuboresha usimamizi katika miradi .

Kaimu mratibu wa TASAF Chalinze, Sostenes Kamguna alibainisha kwamba, vijiji 52 vipo katika mpango huo kiasi cha sh.milioni 947.1 zimetolewa kwa kaya 6,011 huku kaya 3,998 wamepokea kwa njia ya simu .

Kamguna alieleza, milioni 272.190 zimeshatolewa kwa walengwa 563 kati ya 2,517 waliokidhi vigezo.


 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...