Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imeupongeza Umoja wa Falme za Kiarabu (U.A.E) kwa kuendelea kuunga mkono Juhudi za Serikali katika kufadhili miradi mbali mbali ya Maendeleo.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla ametoa kauli hiyo alipokutana na kufanya mazungumzo na Ujumbe wa Umoja wa Falma za Kiarabu (U.A.E) ukiongozwa na Waziri wa Nchi wa U.A.E Sayyid Maythaa Al Shaamy Afisini kwake Vuga Jijini Zanzibar.

Ameeleza kuwa Waziri huyo wa Nchi wa UAE ameihakikishia SMZ kuendeleza mashirikiano katika nyanja tofauti ikiwemo miradi inayowalenga Wanawake na Mayatima.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar amesema Umoja wa Falme za Kiarabu unafahamu juhudi zinazofanywa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kuwatumikia Wananchi wake.

Sambamba na Mhe. Hemed amemueleza Waziri huyo kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inayoongozwa na Rais Dkt. Hussein Ali Mwinyi imeshatoa miongozo ya kukaribisha Taasisi mbali mbali za ndani na za Nje ya Nchi ili kuja kuunga mkono Juhudi hizo.

Pamoja na mambo mengine Mhe. Hemed amemuhakikishia Waziri Maythaa kuwa SMZ itasimamia Misaada wanayoitoa kwa kuwafikia walengwa kama walivyokusudia.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...