Kampuni ya Barrick, kupitia Mgodi wake wa North Mara, imeanza kutekeleza kwa vitendo ahadi iliyotolewa na Rais na Afisa Mtendaji Mkuu wa kampuni hiyo, Mark Bristow la kurekebisha kipande cha barabara korofi katika eneo la vijiji vya Nyamongo na Kewanja wilayani Tarime mkoani Mara, iliyokuwa imeharibika sana na kuleta usumbufu mkubwa kwa wakazi wa eneo hilo wanaotumia barabara hiyo.


Viongozi wa eneo hilo walitoa ombi la kusaidiwa kutengenezewa kipande cha barabara hiyo hivi karibuni wakati walipokutana na Bw. Bristow, alipokuwa nchini hivi karibuni.

Kipande hicho kinachokarabatiwa na Barrick, kina umbali wa kilometa 3.6 kuanzia katika kijji cha Kewanja kwenye kitongoji cha Kwinogo, kuanzia makutano ya barabara ya kwenda Serengeti, hadi kwenye makutano ya barabara ya kwenda Tarime.


Baadhi ya wakazi wa eneo hilo wakiongelea hatua hiyo jana baada ya kushuhudia mkandarasi kampuni ya ujenzi ya Stanley, ameanza kazi ya kuchonga na kumwaga vifusi, walisema kuwa barabara hiyo iliharibika na kuwasababishia usumbufu mkubwa na hasara na walishukuru uongozi wa Barrick kwa ukarabati wa barabara hiyo.


Akiongea kwa niaba ya Wananchi wenzake, Perusi Masiaga Chacha ,mkazi wa eneo hilo alisema ubovu mkubwa wa barabara hiyo ulisababisha kuishi kwa hofu kuitumia hasa watoto wao kuvuka wakati wa kwenda shule, kusababisha kusafiri mwendo mfupi kwa muda mrefu pia kusababisha uharibifu mkubwa wa vifaa vya usafirishaji hasa pikipiki na magari.


Aliishukuru kampuni ya Barrick, kwa kuamua kuwaondolea kero hii ya barabara mbovu ‘’Tunayo furaha kuona barabara hii inatengenezwa kwa kuwa mbali na kuwarahisishia maisha watumiaji wake itasaidia kuchochea maendeleo ya kiuchumi katika maeneo haya yaliyokuwa yanafifishwa na ubovu wa miundo mbinu.Tunaishukuru Barrick, kwa kudhihirisha kuwa mdau mkubwa wa maendeleo katika eneo hili.

Naye Samwel Wambura, akiongea kwa niaba ya madereva wa vyombo vya moto wanaotumia barabara hiyo alisema kuwa kwa muda mrefu imewasababishia hasara kubwa ya kuharibika kwa vyombo vyao na alishukuru Barrick kwa kuona umuhimu wa kuifanyia ukarabati ili iweze kupitika vizuri.

Kwa upande wake, Meneja Mahusiano ya Kijamii wa Mgodi wa North Mara, Gilbert Mworia, alisema barabara hiyo inakarabatiwa kutokana na ombi la viongozi wa eneo hilo pia kutokana na ubovu wake uliosababisha utumiaji wa barabara za mgodini kuwa mkubwa hali ambayo inaweza kuhatarisha maisha ya Wananchi kutokana na barabara nyingi za Mgodini kutumiwa na mitambo mikubwa ya shughuli za uchimbaji.

Kazi ya ukarabati wa barabara korofi katika eneo la vijiji vya Nyamongo na Kewanja,wilayani Tarime ikiendelea








Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...