Meridianbet Tanzania wameendelea na utaratibu wao wa kuwa karibu na jamii, kwa kutoa sapoti kwa vijana katika shughuli zao za kuutafuta mkate wa kila siku. Tumu ya Meridianbet, wikiendi iliyopita iliwatembelea boda boda na kuwaunga mkono katika shughuli zao za utafutaji kwa kuhakikisha wanakuwa salama. Ikiwa ni muendelezo wa kugawa nyenzo za usalama wa boda boda, baada ha kutoa kofia ngumu na reflectors awamu iliyopita, wakati huu wametoa reflector nyingi zaidi kwa vituo vitano vya boda boda.

Vituo ambavyo vilitembelewa na Meridianbet ni Makumbusho, ambapo zoezi hilo lilianza likiongozwa na Twaha Mohammed kutoka ofisi ya masoko ya Meridianbet, aliyeambatana na timu ya watu watatu wengine kutoka kampuni hiyo.



Mwananyamala A, Mwananyamala kwa Kopa, Magomeni, Fire na Muhimbili ni miungoni mwa vituo vilivyonufaika na zoezi hilo la kampuni ya Meridianbet.

Wakati wa shughuli hizi, Meridianbet walisisitiza ni muhimu boda boda kuwa makini na kuzingatia sheria za usalama barabarani kwa ajili ya usalama wao, na wale wanawategemea.

"Tunagawa hizi kwa sababu tunazingatia umuhimu wa usalama wenu, kama vijana na watu ambao mnategemewa na familia zenu na watu wanaowapenda. Tunashauri muendelee kuwa makini barabarani, na kuzingatia sheria za usalama barabarani ambazo zinawahakikishia usalama ninyi na watumiaji wengine wa bara bara." - Twaha Mohammed

"Hawa ni vijana, wanafanya kazi nzuri kujitafutia kipato. Kuwa salama ni jambo la msingi, reflectors zinawasaidia kuonekana zaidi hata wakati wa giza. Sisi kama Meridianbet tunawaunga mkono shughuli zao kwa kuwasaidia kuwa salama zaidi, wakati mwingine tuligawa kofia ngumu, wakati huu tunawapa reflectors. Zoezi hili haliishii hapa." Shadrack Maarufu kutoka kitengo cha masoko Meridianbet.

Boda boda kwa upande wao wanasema wanaona ni jambo jema, na ni faraja kwao kuona wanakumbukwa na kampuni mbali mbali katika masuala ya usalama wao.

"Mimi nawashukuru sana Meridianbet, maana wanazingatia kuwa sisi vijana tunahitaji kuwa salama. Tunafarijika sana, natoa shukrani kwa niaba ya wenzangu. Na mida ya kubeti imewadia nitaenda kuchakata majamvi yangu"

Meridianbet ni kampuni kongwe ya ubashiri, wanaokuhakikoshia huduma bora za ubashiri wa mtandaoni na Kasino za mtandaoni. Cheza michezo yote ya kasino mtandaoni, michezo ya virtual na ubashiri wa matukio mbali mbali yamichezo ulimwenguni na Meridianbet. Bila kusahau una nafasi kibao za kushinda Jackpot za kasino ya mtandaoni ya Meridianbet.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...