Tayari Pesapal inafanya biashara Kenya na Uganda ambako inazihudumia zaidi ya biashara ndogo na za kati 50,000. Dira yake ni kuziwezesha nchi za Kiafrika kutoa huduma za kifedha za kidijitali zenye bei nafuu, salama na zinazozingatia mahitaji ya soko husika kwa ajili ya kuchochea ukuaji uchumi endelevu.
“Kuweza kupenya na kupanua shughuli zake nchini Tanzania ni hatua kubwa ya kimkakati yenye tija kwa Pesapal, ambayo ina matarajio ya kufanya vizuri sokoni na kuwawezesha Watanzania kupata thamani kutoka kwenye suluhisho za kifedha bunifu za kidijitali zilizosalama na zenye manufaa makubwa,” kampuni hiyo ilisema katika taarifa kwa vyombo vya habari.
Akizungumzia kupatikana kwa leseni hiyo, Mkurugenzi Mkuu wa Pesapal Tanzania, Bi Bupe Mwakalundwa, alisema kupatikana kwa leseni hiyo kutaiwezesha kampuni yao kupanua wigo wa upatikanaji wa bidhaa zao barani Afrika.
Kama ilivyo BoT, alifafanua, Pesapal ni muumini wa matumuzi ya teknolojia kuchochea ukuaji wa uchumi na maendeleo ya huduma jumuishi za kifedha.
“Kwetu sisi Pesapal, lengo letu ni kuimarisha teknolojia ili kutengeneza suluhisho za malipo zinazorahisisha jinsi wateja na baishara mbalimbali wanavyolipwa,” alisema.
Bi Bupe aliongeza kuwa Pesapal inataka kuwapa Watanzania fursa ya kupata huduma bunifu za kifedha na kidijitali ambazo zinafaa kwa kada na biashara zote.
Wanufaika wengine wa uwekezaji huo watakuwa ni wafanyabiashara wa mtandaoni, watu binafsi, na wale wote ambao kwa sasa hawajafikiwa na mifumo rasmi ya kawaida ya malipo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...