Mfano wa kifaa cha kupimia afya ya udongo
**
Na Mwandishi wetu - Mwanza
Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI) Ukiriguru imewataka Maafisa Ugani kutoka kwenye Halmashauri za wilaya kwenda kupigwa msasa kwenye kituo hicho jinsi ya kutumia vifaa vya kupimia udongo (Soil Test Kit) walizopewa kwa ajili ya kupima afya ya udongo kwenye maeneo yao.

Akizungumza kwenye maonesho ya Nane Nane yanayoendelea katika viwanja vya Nyamhongolo jijini Mwanza ,Mtafiti kutoka Idara ya Udongo TARI Ukiriguru, Hainess Msuya amesema endapo maafisa ugani hawatapata mafunzo Soil Test Kit hiyo haitaleta matokeo yanayotarajiwa.

“Maafisa ugani waje wapewe semina ya jinsi ya kutafsiri taarifa zinazopatikana baada ya kupima udongo kuna uhakika wengi wao itakuwa vigumu kutafsiri taarifa hizo kutokana na ukweli kwamba wengi wametoka Chuo siku nyingi na wengine hawajawahi hata kukutana na hizo Soil Test Kit",amesema Mtafiti huyo.

Mtafiti huyo alisema tunapima udongo ili kujua afya ya udongo na vipimo hivyo ndiyo vitatusaidia kwenye eneo husika ni nini tunahitaji kupanda na ni mbolea gani tuweke kwenye udongo huo

“Vifaa ni vizuri nashauri Halmashauri ziwapeleke maafisa ugani kwenye vituo vya TARI wapewe mafunzo ya muda mfupi. Huku Kanda ya Ziwa Magharibi waje Ukiriguru na wa Kanda zingine waende kwenye vituo vya TARI vilivyopo kwenye maeneo yao ili wawahi msimu wa mvua huu kabla ya kilimo kuanza”,amesema

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...