Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalumu, Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima ameipongeza benki ya NMB kwa kutenga fedha kwaajili ya mikopo ya machinga na pia kuweka huduma zitakazorahisisha utendaji kazi wa kundi hili la wafanyabiashara wadogo.

Waziri Gwajima ameyaeleza hayo alipotembelea soko la machinga la old airport jijini Mbeya na kujionea hali halisi ya Biashara za machinga katika soko hilo ambalo machinga wamehamia tangu mwaka 2020.

Mhe waziri aliipongeza benki ya NMB kwa kutenga kiasi cha Bilioni 200 kwaajili ya kuwakopesha machinga jambo ambalo litawasaidia kujikwamua kiuchumi.

Naye Mwenyekiti wa shirikisho la Umoja wa Machinga Tanzania (SHIUMA), Ndugu Ernest Matondo Masanja aliishukuru Benki hiyo pia kwa kuanzisha rasmi kadi za ATM maalumu kwa machinga huku akiwasihi machinga wote nchini kuunga mkono juhudi za Benki hiyo kuwainua kiuchumi.

Lakini pia, Meneja wa Benki ya NMB kanda ya Nyanda za Juu, Straton Chilongola alitumia fursa hiyo kuwakumbusha wamachinga kuwa licha ya huduma bora ambazo NMB inatoa, lakini pia, wanaweza kujikatia bima mbalimbali ikiwemo bima maalumu kwaajili ya Machinga ambayo itawafanya wafanye shughuli zao kwa kujiamini na kutokuwa na hofu kwani itokeapo janga lolote basi Bima itafidia.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...