Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Czech, Mhe. Martin Tlapa amewasili nchi leo kwa ziara ya kikazi ya siku tatu kuanzia tarehe 2 hadi 4 Oktoba 2022.

Mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Jijini Dar es Salaam, Mhe. Tlapa amepokelewa na Mkurugenzi wa Idara ya Amerika na Ulaya, katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Swahiba Mndeme na Balozi wa Tanzania nchi Ujerumani ambaye pia anawakilisha Jamhuri ya Czech, Mhe. Dkt. Abdallah Possi.

Akiwa nchini, Mhe. Tlapa kwa nyakati tofauti, atakutana kwa mazungumzo na Waziri wa Nchi-Tamisemi, Waziri wa Afya, Waziri wa Viwanda na Biashara, pamoja na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Wengine ni Mkurugenzi Mkuu wa Bohari Kuu ya Dawa (MSD) pamoja na Mkurugenzi wa Ununuzi na Ugavi wa Hospitali ya Jeshi la Wananchi (JWTZ).

Tanzania na Czech zimekuwa zikishirikiana katika sekta za elimu,utamaduni, afya, biashara na uwekezaji.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Czech, Mhe. Martin Tlapa amewasili nchi kupitia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Jijini Dar es Salaam
Balozi wa Tanzania nchi Ujerumani ambaye pia anawakilisha Jamhuri ya Czech, Mhe. Dkt. Abdallah Possi (wa kwanza kushoto) akimueleza jambo Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Czech, Mhe. Martin Tlapa walipokuwa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Idara ya Amerika na Ulaya, katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Swahiba Mndeme akimueleza jambo Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Czech, Mhe. Martin Tlapa walipokuwa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Czech, Mhe. Martin Tlapa akiteta jambo na Mkurugenzi wa Idara ya Amerika na Ulaya, katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Swahiba Mndeme

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...