Na Shamimu Nyaki

Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Pauline Gekul amesema Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan inaendelea kuibua na kukuza vipaji kupitia sekta zake.

Mhe. Gekul amesema hayo katika Mkutano wa Hadhara wa Rais Mhe. Samia uliofanyika leo Novemba 23, 2022 katika Uwanja wa Kwaraa mjini Babati ambapo amesema Takriban  Shilingi bilioni 2 zimetengwa kwa mwaka huu wa fedha kwa ajili ya Mfuko wa Utamaduni na Sanaa.

"Halmashauri ya Mji wa Babati imetumia takriban Shilingi milioni 95 kujenga uzio katika Uwanja  huu wa Kwaraa mjini hapa, naomba nitumie nafasi hii kutoa wito kwa Halmashauri zote nchini kutenga fedha za mapato ya ndani  kwa ajili ya kukarabati na kujenga  miundombinu ya michezo", amesema Mhe. Gekul.

Ameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita, kwa kutenga fedha takriban Shilingi bilioni 300 kwa ajili ya kusaidia timu za Taifa  ambazo zimesaidia timu ya Taifa ya Walemavu ya Tembo Worrios na Timu ya Taifa ya Wanawake chini ya Miaka 17 (Serengeti Girls) ambazo zote zimefuzu Kombe la Dunia na kufika hatua ya Robo Fainali.



 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...