Na Mwamvua Mwinyi,Pwani


Kiwango cha maambukizi ya ugonjwa wa Ukimwi na Vifo vitokanavyo na ugonjwa huo ,mkoani Pwani kimeshuka kutoka asilimia 5.9 hadi kufikia asilimia 5.5.

Akitoa hali ya kiwango Cha maambuzi ya ugonjwa huo, katika maadhimisho ya siku ya Ukimwi Duniani Mkoani Pwani yaliyofanyika viwanja vya shule ya msingi Mtongani, Kibaha ,mwakilishi wa mkuu wa mkoa huo ,mkuu wa wilaya ya Kibaha Sara Msafiri, alieleza kiwango hicho kimeshuka kati ya kipindi cha mwaka 2012 hadi 2017.

Alieleza ,mbali ya mafanikio hayo Halmashauri ya Kibaha Mjini , Mkuranga na Chalinze bado zina maambukizi makubwa kutokana na changamoto ya muingiliano wa idadi ya watu wanaotoka nje ya halmashauri hizo.

Aidha ,Sara alieleza kundi la vijana pamoja na wanaume wanaonekana kuwa na mwamko mdogo wa kujitokeza kupima afya zao.

Alifafanua , katika kipindi cha mwezi January Hadi Novemba mwaka huu takwimu zinaonyesha ,kuna maambukizi mapya ya vijana 1,004 wenye umri kati ya miaka 15-24 .

"Kauli mbiu ya maadhimisho haya ni IMARISHA USAWA, Lazima tuweke usawa ,unaweza kuona vijana hawa ni wadogo ,Lakini tukumbuke umri huu ni wa kukua ,na ndio wanaojiingiza katika maadili yasiyo mema ikiwemo madada poa,wavuta bangi na madawa ya kulevya hivyo kujikuta wakipata maambukizi ya virusi hivyo"alisema Sara.

Awali muathirika wa VVU kutoka kata ya Kikongo, Elizabeth Ngonyani alieleza ,kuugua Ukimwi sio kufa kwani tangu agundulike kuwa na ugonjwa huo ,na wapo waliokufa na kumuacha yeye akiwa afya njema.

Nae dkt. Sisty Moshi kutoka THPS alieleza ,THPS inafadhiliwa na Serikali ya Marekani na inashirikiana na mkoa huo kwa miaka kumi Sasa .

Alisema kiwango Cha upimaji mkoa upo kiwango Cha asilimia 95 na walio kwenye dawa za kufubaza VVU ni takriban watu 50,000 sawa na asilimia 98.

Moshi alieleza, kwa mwaka huu wametoa fedha Bilioni 3.2 kwa ajili ya shughuli za Halmashauri .

Kaimu Katibu Tawala mkoani Pwani,Rukia Mhango aliishukuru THPS ,AMREF na wadau wengine wa jamii kwa kuboresha Mazingira ya utoaji huduma za kiafya .

Aliwaasa ambao wamegundulika na VVU na kuanza dawa za kufubaza virusi vya Ukimwi wasiache dawa na wasiwe watoro kufuata dawa na kuhudhuria kliniki zao.




 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...