Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo Dkt Juma Ramadhan
HOSPITALI
ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo inatarajia kuanzisha huduma za Kliniki za
Kibingwa wakati wa muda wa ziada wa jioni itakayoanza kuanzia Aprili 9
mwaka huu katika hospitali hiyo.
Akizungumza leo Kaimu Mganga
Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo Dkt Juma Ramadhan
amesema huduma hizo zitaaza saa tisa na nusu jioni mpaka muda ambao
wagonjwa watamalizika ambao watapata fursa ya kuonana na madaktari
bingwa waliopo kwenye hospitali hiyo.
Dkt Juma alisema kwamba
katika kliniki hiyo huduma mbalimbali za kibingwa ikiwemo magonjwa ya
ndani,magonjwa ya ya upasuaji,magonjwa ya wakina mama,magonjwa ya
watoto,magonjwa wa koo,pua pamoja na sikio .
Aidha alisema
kwamba huduma hizo zitatolewa kwa wagonjwa wote wenye bima bila kujalia
aina gani ya bima lakini pia wale wagonjwa wanaofanya malipo ya keshi
yatapokelewa.
Hata hivyo alisema huduma hiyo itatolewa siku Jumatatu mpaka Ijumaa kuanzia saa tisa na nusu mpaka pale watakapomalizika.
Dkt
Juma aliwahimiza wananchi wa mkoa wa Tanga kujitokeza kwa wingi
kuhudhuria kliniki hizo ili kuweza kukutana na madaktari bingwa wa
hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga
Hata alisema uwepo wa
kliniki hiyo utasaidia kutoa fursa kwa wagonjwa kuweza kukutana na
madaktari bingwa ambao wataweza kuwasaidia hivyo watumie nafasi hiyo
kuweza kuonana na madaktari hao bingwa waliopo kwenye hospitali hiyo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...