Na Mwandishi Wetu

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu imeiagiza Wakala wa Ujenzi Tanzania (TBA), kuwaondoa wapangaji ambao hawalipi kodi ya nyumba, hususani watumishi wa taasisi za serikali.

Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Seleman Kakoso alitoa agizo hilo jana jijini Dar es Salaam wakati kamati hiyo ilipotembelea mradi wa nyumba za makazi ya watumishi wa umma eneo la Temeke.

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kutembelea mradi huo, Kakoso alisema TBA wanapaswa kuwachukulia hatua watumishi waliopanga katika nyumba zao kwa kuowaondoa pasipo kuwaonea huruma.

"Watumishi wa serikali walipe kodi wasikae bure. Waziri nenda kawasaidie TBA kuwaondoa wapangaji sugu wasiolipa kodi. Tunataka TBA ijitegemee isitegemee ruzuku kutoka kwa serikali, " alisema Kakoso.

Mbali na kutoa agizo hilo, Kakoso aliitaka TBA kuajiri watumishi zaidi ili waweze kufanya kazi kwa weredi kwa sababu taasisi hiyo ina upungufu ya watumishi zaidi ya 500.

Pia, aliiagiza TBA kujiendesha kibiashara, wawe na vyanzo vya mapato vitakavyokuwa endelevu.

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya maagizo hayo, Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa alisema wameyapokea maelekezo na wanakwenda kuyafanyia kazi.

Kuhusu watumishi kulipa kodi ya nyumba, Profesa Mbarawa aliwataka Watanzania kuwa na tabia ya kulipa kodi kwa wakati ili kupeusha usumbufu wa kuondolewa.

Alisema kwa sasa TBA wanaandaa mfumo wa smart lock utakaowazuia wapangaji sugu kukwepa kulipa kodi ya nyumba.

"Kwenye nyumba hizi na zingine zote nchini tunakwenda kuweka mfumo wa smart lock. Kama mtu hujalipa kodi huingii ndani," alisema Profesa Mbarawa.

Naye Mtendaji Mkuu wa TBA, Daud Kondoro, alisema mradi huo unajengwa wa gharama ya Sh.bilioni 19.4 ambpao kwa sasa umefikia 15 na utatekelezwa kwa miaka miwili.

Mtendaji Mkuu Kondoro ameongeza kuwa mradi huo unakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwamo mabadiliko ya hali ya hewa hususani nyakati za mvua, wizi wa vifaa mbalimbali vya ujenzi hali inayosababisha kucheleweshwa kwa utekelezaji.

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu iko jijini Dar es Salaam ambapo inapokea taarifa na kukagua maendeleo ya miradi inayotekelezwa na Taasisi za Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi.




Muonekano wa hatua iliyofikiwa ya ujenzi wa jengo la watumishi wa Umma linalojengwa na Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) Temeke mwisho, jijini Dar es Salaam. Ujenzi wa Jengo hilo umefikia asilimia 15 na unatarajiwa kukamilika ndani ya miaka miwili.PICHA NA WUU



Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA), Arch. Daud Kondoro akiwasilisha taarifa kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, kuhusu maendeleo ya ujenzi wa nyumba za watumishi Temeke mwisho, wakati kamati hiyo ilipotembelea mradi wa ujenzi wa nyumba za watumishi Temeke Mwisho, jijini Dar es Salaam.



Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Tanga Mjini na Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu Mhe. Mhandisi Mwanaisha Ulenge akisisitiza Jambo kwa Uongozi wa Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi na Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) hawapo pichani, wakati kamati hiyo ilipotembelea mradi wa ujenzi wa nyumba za watumishi Temeke Mwisho, jijini Dar es Salaam.



Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa akifafanua jambo kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu mipango ya Serikali katika ujenzi wa nyumba za watumishi, wakati kamati hiyo ilipotembelea mradi wa ujenzi wa nyumba za watumishi Temeke Mwisho, jijini Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...