Catholic Relief Services (CRS) inajivunia kutangaza mwaka wake wa 60 wa kuwepo nchini Tanzania. Ili kuadhimisha hatua hii muhimu, CRS inaandaa hafla mnamo Machi 28 kuwakaribisha viongozi wa serikali ya Tanzania, viongozi wa makanisa, mashirika washirika, wafadhili, na wafanyakazi wa sasa na wa zamani wa CRS nchini Tanzania. Sean Callahan, Rais na Mkurugenzi Mtendaji wa Catholic Relief Services, atajumuika kwenye hafla hii itakayofanyika Dar es Salaam-Tanzania.

Akizungumzia tukio hilo, Callahan alisema “wakati CRS duniani inatimiza miaka 80, ni heshima kubwa kuwapo Tanzania kwa miaka 60, tukifanya kazi bega kwa bega na Kanisa Katoliki, washirika wetu wa maendeleo na jumuiya tunazohudumia, na kazi hii inaendelea kuwa jukumu kubwa kwetu kutokana na uaminifu tuliopewa."

CRS imekuwa ikihudumia jumuiya za Kitanzania tangu 1962. Wakati ambapo mahitaji ya kibinadamu yamefikia kiwango cha juu zaidi duniani, tunaendelea kuunga mkono mabadiliko yanayochochewa na jamii kwa kiwango kikubwa nchini kwa kufanya kazi bega kwa bega na viongozi wa dini mbalimbali, washirika wa kitaifa na jamii mbalimbali katika njia yao ya ustawi na ustahimilivu dhidi ya athari mbaya za changamoto kuu za leo, ikiwa ni pamoja na masuala ya jinsia, upatikanaji wa masoko na fedha kwa vijana, uhaba wa chakula na mabadiliko ya hali ya hewa.

Maadhimisho ya miaka 60 ya CRS Tanzania yataanza Machi 28 kwa Misa ya Shukrani katika Kanisa la Mtakatifu Petro lililopo Oysterbay saa 8:00 Mchana, baada ya misa, jumuiko la pamoja limeandaliwa katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam na kutakuwa na shughuli na maonyesho mbalimbali, ikiwa ni pamoja na ukuta wa kumbukumbu unaoonyesha mafanikio makubwa ya CRS kwa miaka 60 iliyopita nchini Tanzania, maonyesho ya programu za sasa na zilizopita na hotuba kutoka kwa Rais wa CRS, Meneja CRS Tanzania, kiongozi wa kanisa, na kiongozi wa serikali pamoja na shuhuda kutoka kwa wafanyakazi na washirika, na uwasilishwaji wa ushairi wa kisasa. Katika kuunga mkono dhamira ya Wizara ya Afya ya Tanzania ya kuhakikisha afya na ustawi wa raia wote wa Tanzania katika mapambano dhidi ya COVID-19, CRS itawezesha banda la chanjo ya COVID-19 katika hafla hiyo.

Catholic Relief Services (CRS) imekuwa ikifanya kazi na watu wanaoishi katika mazingira magumu zaidi katika jamii za vijijini nchini Tanzania tangu mwaka 1962. Leo, programu ya nchi hii inasaidia miradi ya afya, lishe na maendeleo ya utotoni, ushirikishwaji wa kijinsia, uwezeshaji vijana na ujasiriamali, mabadiliko ya tabianchi, pamoja na maji, na usafi wa mazingira(WASH).

Kwa habari zaidi, tembelea https://www.crs.org/our-work-overseas/where-we work/tanzania Catholic Relief Services (CRS) ni wakala rasmi wa kimataifa wa kibinadamu wa jumuiya ya Kikatoliki nchini Marekani. Shirika hili linapunguza umasikini na kutoa msaada kwa watu wanaohitaji msaada katika zaidi ya nchi 100, bila kujali rangi, dini au utaifa. 

Kazi ya misaada na maendeleo ya CRS inakamilishwa kupitia programu za kukabiliana na dharura, VVU, afya, kilimo, elimu, fedha na kujenga amani. Kwa habari zaidi, tembelea www.crs.org

Rais wa Shirika la Misaada ya Kibinadamu la Katoliki la Marekani (Catholic Relief Services) Sean Callahan (katikati), Matt Davis, Mkurugenzi wa CRS Kanda ya Afrika Mashariki (wa kwanza kushoto) na Kellie Hynes, Mkurugenzi Mkaazi wa CRS nchini (wa kwanza kulia) wakikata keki kusheherekea miaka 60 ya asasi hiyo kwenye hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam tarehe 28 Marchi 2023.
Marilyn Helen Chottah, Mkuu  wa Ofisi ya CRS Mbeya, akitoa maelezo kwa waandishi wa habari wakati wa maadhimisho ya miaka 60 ya CRS jijini Dar es Salaam Machi 28







.
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...