Na Mwandishi wetu, Michuzi Tv

MTANDAO wa jinsia Tanzania (TGNP) wakishirikiana na Internews kupitia Mradi wa Boresha Habari watoa mafunzo kwa Wanachuo wanaosoma Masomo ya Uandishi wa habari katika Chuo Kikuu Cha Huria Tanzania ili waweze kuwa na jicho la kijinsia kwenye habari.

Akizungumza jijini Dar es Salaam leo Machi 23, 2023 na waandishi wa habari, Mwezeshaji kutoka Mtandao wa jinsia Tanzania (TGNP), Deogratius Temba amesema kuwa lengo la ni kuwaweka waandishi wa habari sehemu nzuri mapema kabla hawajawa na msongamano wa majukumu pale watapomaliza chuo.

“Tunataka waandishi waweze kuzingatia usawa wa kijinsia katika Uandishi wa habari mbalimbali katika jamii.”

Amesema zipo habari nyingi kwenye jamii ambazo hazijaandikwa kuhusiana na wanawake pamoja na makundi ya watu wenye ulemavu ambazo zinaonekana hazina maana katika uuzaji kwenye vyombo vyao vya habari.

“Habari hizo ndizo tunazojaribu kuwaeleza waandishi wa habari vijana ili wajue ni namna gani wanazipa kipaumbele wanapokuwa wanafanya kazi zao.” Ameeleza Temba

Amesema kuwa ili kuleta maendeleo lazima habari ziwe zuri na ziweze kuandikwa kwa kukwepa uzalilishaji wowote wa jinsi ya ME au KE ili kuleta maendeleo katika shughuli zozote za maendeleo.

Amesema kuwa habari inayozingatia sauti za jinsi zote mbili ya wanawake na wanaume .

Kwa upande wa Mratibu wa mafunzo wa Mradi wa Boresha Habari kutoka 'Internews', Mariam Oushoudada amesema mafunzo hayo yataenda kusaidia wanafunzi katika kuhakikisha kunakuwa na uwiano wa uongozi katika tasnia ya habari.

"Mafunzo haya tumeona tuyatoe kwa wanachuo wakiwa chuoni yaani mwanzoni kabisa ili wawe na uelewa wa masuala ya jinsia pale wanapo andika habari katika vyombo vyao vya habari pale watapomaliza masomo." Amesema Mariam.

Amevitaj vyuo ambavyo vitanufaika na mafunzo hayo kuwa ni Chuo Kikuu cha Tumaini, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) ,Chuo Kikuu Huria cha Tanzania, Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustino(SAUT) na Practical School of Journalism.

Amesema Mradi huo utatanua uelewa wa jamii kuhusiana na usawa wa kijinsia pamoja na kutoa uelewa kwa waandishi wa habari chipukizi ili waweze kuandika na kuzipa kipaumbele habari za jinsia.

Amesema mafunzo hayo yatakuwa endelevu pia kutakuwa na atamizi kwaajili ya kuendelea kuwa nao pamoja ili waweze kuandika habari ambazo zitakuwa na usawa wa kijinsia bila kukandamiza jinsi yeyote katika jamii.

Kwa upande wa Mwezeshaji kutoka TGNP Ester Wilium amesema mafunzo hayo yanawajengea uelewa waandishi wa habari chipukizi kuweza kuandika habari ambazo hazipendelei na zinaangalia jinsi zote ‘Mwanamke na mwanaume’ ili uandishi wa habari wa sasahivi uwe tofauti na uandishi wa zamani.

Kwa upande wa mnufaika wa mafunzo hayo, kutoka Chuo Kikuu Huria Tanzania, Aniva Mwongola amesema kuwa mafunzo hayo atayafanyia kazi kwa vitendo kwani kumekuwa na changamoto ya waandishi kuandika habari ambazo hazina sauti za jinsia zote.

“Mafunzo haya yamenijengea uelewa wa masuala mapana na namna ambavyo nitaweza kuisaidia jamii kuelewa uhalisia wa jinsia hasa ukiangalia masuala ya kutambua haki ya kila mwanadamu na kupata fursa mbalimbali.” Amesema Aniva

Akizungumzia fursa hizo amesema kila mwanadamu anatakiwa kupata fursa za kiuchumi, Uongozi na fursa za elimu, amesema ingawa serikali imewezesha jamii kupata fursa mbalimbali lakini kama mwandishi wa habari anafursa ya kufanya kwa nafasi yake ili kuwe na usawa katika jamii kwa ujumla.
Mwezeshaji kutoka Mtandao wa jinsia Tanzania (TGNP), Deogratius Temba akizungumza na wanachuo Kikuu Huria cha Tanzania wakati wa kutoa mafunzo ya usawa wa kijinsia wakati wa kuripoti habari. Mafunzo hayo yamefanyika jijini Dar es Salaam leo Machi 23, 2023.
Mratibu wa mafunzo wa Mradi wa Boresha Habari kutoka 'Internews', Mariam Oushoudada akizungumza na wanachuo Kikuu Huria cha Tanzania wakati wa kutoa mafunzo ya usawa wa kijinsia wakati wa kuripoti habari. Mafunzo hayo yamefanyika jijini Dar es Salaam leo Machi 23, 2023.
upande wa Mwezeshaji kutoka TGNP Ester Wilium akizungumza na wanachuo Kikuu Huria cha Tanzania wakati wa kutoa mafunzo ya usawa wa kijinsia wakati wa kuripoti habari. Mafunzo hayo yamefanyika jijini Dar es Salaam leo Machi 23, 2023.
Baadhi ya wanachuo Kikuu Huria cha Tanzania wakiuliza maswali wakati wa mafunzo ya uandishi wa habari za jinsia kutoka Mtandao wa Kijinsia Tanzania (TGNP) wakishirikiana na Internews kupitia Mradi wa Boresha habari. Mafunzo hayo yamefanyika jijini Dar es Salaam leo Machi 23, 2023.




Baadhi ya wanachuo Kikuu Huria cha Tanzania wakipata mafunzo ya uandishi wa habari za jinsia kutoka Mtandao wa Kijinsia Tanzania (TGNP) wakishirikiana na Internews kupitia Mradi wa Boresha habari. Mafunzo hayo yamefanyika jijini Dar es Salaam leo Machi 23, 2023.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...