Na Mwamvua Mwinyi,Rufiji
WANANCHI  waliovamia Eneo la Hifadhi la Chemchem ya Maji ya Moto Rufiji- wamegewa Eneo kwenye hifadhi hiyo.


Hayo yalibainishwa na Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge wakati akitoa tamko la kuhitimisha Mgogoro huo ikiwa ni Utekelezaji wa maazimio ya Baraza la Mawaziri iliyotokana na Kamati ya Mawaziri wa nane wa Kisekta walioshughulikoa migogoro hiyo.

Akitoa maagizo hayo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa, Major Edward Gowele Mkuu wa Wilaya ya Rufiji- amewataka Wananchi wanaozunguka maeneo hayo kutovamia eneo hilo na kuagiza Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania TFS na Kamshna Msaidizi wa Ardhi kupima upya eneo hilo la Hifadhi na kuandaa GN Mpya.

Aliwataka TFS kuchonga Barabara kuzunguka eneo hilo ili Kuweka Kinga kati ya Wananchi na Hifadhi.

Katika Hatua Nyingine alitembelea Delta ya Mto Rufiji- na kuhitimisha Mgogoro wa Ardhi uliopo la Wananchi kuendesha shughuli za kibinadamu katika hifadhi hiyo ya Misitu ya Mikoko na mazalia ya Samaki .

Akimwakilisha Mkuu wa Mkoa kwenye Kuhitimisha Mgogoro huo Mkuu wa Wilaya ya Kibiti, Col Samwel Kolombo alipiga marufuku ukataji wa Misitu ya Mikoko ovyo.

Aidha alimtaka Mkurugenzi wa Halmshauri ya Kibiti kutoa Elimu ya uhifadhi wa Wananchi na kuwawezesha vifaa vya kuvulia samaki kwenye Maji marefu.

Alisisitiza pia kuanzisha kwa vikundi vya uhifadhi BMU ili kuimariasha ulinzi wa hifadhi hiyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...